YATAKAYOJIRI LEO JIJINI MWANZA KATIKA SIKU YA WANAWAKE

MH. VICKY KAMATA KUTOA BURUDANI TAMASHA LA KUONGEZA MAARIFA KUFANYIKA, MARCH 8, SIKU WANAWAKE DUNIANI KATIKA UKUMBI WA GOLD CREST JIJINI MWANZA!!
Tamasha la kuongeza maarifa, linatarajiwa kufanyika machi 8 mwaka huu, ikiwa ni siku ya wanawake duniani.

Tamasha limeandaliwa na akina dada kutoka kundi la Bedefesera hapa jijini Mwanza na litafanyika kwenye hoteli iliyo na hadhi ya kimataifa ya Gold crest.
Unajua utapata maarifa gani siku hiyo? Karibu uungane, kwa kununua kadi yako ya Tsh 30,000/= itakayokuwezesha pia kupata chakula cha jioni na vinywaji laini. Piga simu namba 0683962902 kwa manunuzi ya kadi yako.

Bedefesera inaundwa na watangazaji mahiri hapa nchini, akiwemo Rahab fred, Beatrice Rabach, Felister Kulwijira, Deborah Mpagama, Erica Elias na Seda Ilija.

 Mwenyekiti wa kikundi hicho Rahab Fred, amesema Tamasha litatoa mafunzo ya Ujasiriamali, Malezi ya Familia, Afya na jinsi ya kuweza kupata mikopo kwa masharti nafuu.

Burudani kabambe inatarajiwa kutolewa na mbunge wa viti maalum kutoka Geita Mh. Vick Kamata, pamoja na wasanii wengine maarufu kibao

Kazi kwenu wadau kuhudhuria tamasha hilo, hakika Blog hii, inawatakia mafanikio mema katika mwanzo mzuri wa kuongeza maarifa kwa wanajamii...Bigup Bedefesera!!!!!

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA