GHARAMA ZA MATIBABU VYUONI NI MRADI WA VYUO HUSIKA?

MAKALA HII IMEANDALIWA NA 
ANTHONIUS CLEMENT
Mwanafunzi wa chuo kikuu cha mt.Augustino anayesomea shahada ya mahusiano ya Umma na Masoko mwaka wa pili.
Email:tonyboy1989@yahoo.com
Mobile: + 255 717437729 /+255762 963674

Wengi wetu tunafahamu  juu ya umuhimu wa Afya katika jamii yoyote ile. Jamii yenye Afya bora ndiyo yenye maendeleo makubwa kijamii na hata kiuchumi. Nakatika  suala hili siwezi kusita kumzungumzia mwanazuoni  anayea julikana  kama Vans Parkard mwanazuoni huyu wa saikolojia na masomo ya sayansi ya jamii na hasa mawasiliano aliweza kuanisha mahitaji makuu nane ya mwanadamu, Moja ya hitaji hilo ni hitaji la kuishi muda murefu (Imotarity needs).
 
Hitaji hili ndilo linalo wafanya watu wahangaike kwa muda mrefu waki jipodoa ilimradi tu waonekane bado vijana wabichi. Mwaka mmoja nanusu uliopita Watanzania tuliweza kushuhudia wananchi wengi wakifurika katika kitongoji cha Semunge huko Loliondo alimaarufu “ kwenye kikombe cha babu”hii inadhirisha umuhimu wa  kuwa na Afya na siha njema  kwa ujumla.
 
Hapa nchini Tanzania  dhamana ya  afya  imewekwa chini ya taasisi muhimu inayo shughulikia huduma za afya kwa kuwasaidia wamanchi wote kupata huduma za Afya kwa gharama nafuu kabisa.Taasisi hii inajulikana kama Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya .
 
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulianzishwa mahususi chini ya sheria ya ya bunge namba 8 ya mwaka 1999 sura namba 395 toleo la mwaka 2002.Bima ya Afya ilianzishwa mahususi kwaajiri  ya kukidhi hitaji la usalama wa Afya kwa watanzania wote nakwa kuanza ilianza kuwa hudumia watu waliopo katika  sekta rasmi za kazi na kufuatia mabadiliko ya sheria hivi sasa Mfuko wa Taifa wa bima ya Afya  unahusisha hata watu wasio katika sekta rasimi kupitia Mfuko  wa Afya ya Jamii (CHF)
 
Kwakuona kuna baadhi ya ya makundi yameachwa na  na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ulianzishwa utaratibu wa  kutoa matibabu kwa wanafunzi wa  elimu ya juu. Utaratibu huu unalenga  kuwapa Bima ya Afya  wanafunzi wa  vyuo vya elimu ya juu popote nchini ambapo humwezesha  mwanafunzi kupata  huduma za matibabu wakati wote awapo masomoni nawakati wa likizo katika muhula husika.
 
Chini ya utaratibu wa  Mfuko wa Taifa wa bima ya Afya chuo husika huwaandikisha wanafunzi wake kama mdhamini  wa wanfunzi hao,pia kunamkataba wa maridhiano baina  na Mfuko  waTaifa wa bima ya Afya ,vilevile mkataba baina ya mwanafunzi na  na bima ya afya (NHIF)niwa kipindi cha miaka mitatu na hurejewa kila mwaka .pia baada ya  mwanafunzi kuhitimu chuo huwa na jukumu la kurudisha kadi ya uanachama kwani mkataba na mwanfunzi husika huwa umekwisha.
 
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) pamoja na kuingia mkataba kati ya chuo na mwanafunzi umetoa mchanganuo juu ya namna gani michango ina wasilishwa,mchanganuo huo ni  kama ifuatavyo: Mwanafunzi hulazimika kuchangia shilingi za kitanzania 4,200 kwa mwezi sawa na shilingi 50,400 kwa mwaka!mwanafunzi akisha changia  mchango  atapata matibabu kwa  kipindi chote cha mwaka wa masomo pia hata awapo likizo. Ifahamike hapa kuwa  kuna baadhi ya wanafunzi wana bima za Afya hivyo utara tibu huu wao hauwahusu kwani wao tayari ni wanchama na wana vitambulisho vyao na wanapata huduma za matibabu kama kawaida.
 
Baadhi ya vyuo hapa nchini vimeshindwa kuridhia makubaliano ya mkataba kati yake na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, hapa Hapa maswali mengi yanaweza kuzuka labda ni mradi wa vyuo husika? ni kwanini vyuo hivi vinashindwa kuridhia makubaliano na mfuko huu wenye lengo la kutoa huduma za kiafya kwa Watanzania wote nchini na kwa gharama nafuu.
Kwa mfano chuo cha Mtakatifu Agustino kinao  utaratibu wa kila mwanafunzi kulipia shilingi 100,000 kila mwaka kwaajiri ya matibabu pindi awapo masomoni lakini bado huduma zinazo tolewa ni duni na hazikizi mahitaji,vilevile mwanfunzi  pindi auguapo  wakati wa likizo hulazimika kujigharimia yeye mwenyewe gharama za matibabu!!
 
Ukiondoa chuo Kikuu cha Dodoma ambacho wanafunzi hulipia shilingi 100,00 nakupewa huduma za matibabu kwa miaka yote mitatu,Pia  chuo cha CBE navingine vingi vina utaratibu kama huo ambapo mwanafunzi hulazimika kulipa zaidi ya  shilingi 90,000 kila mwaka kwaajiri ya matibabu.Kwa mifano hii tunaweza kuona ni jinsi gani wanafunzi wa baadhi ya vyuo vikuu hapa nchini wanakumbana na adha ya matibabu pindi wauguapo aidha wakiwa masomon, pia wakati wa  likizo hulazimika kuji gharimia wenyewe matibabu.
 
Ukilinganisha na vyuo hapa nchini kama,Chuo Kikuu cha Dar-es salaam,SUA,pamoja na Mzumbe vyuo hivi tayari vimekwisha ridhia mkataba na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na Wanafunzi wa vyuo hivi hupata matibabu pindi wawapo masomoni nahata wakati wa likizo kwa gharama ya shilingi 50,400 tu kwa mwaka mzima.
 
Binafsi najiuliza  kwanini baadhi ya vyuo havijaridhia kuingia mkataba na Mfuko wa Taifa wa  Bima ya Afya ili kuwapunguzia  gharama za matibabu wanafunzi hawa ambao wengi wao wanatoka katika familia zenye kipato cha chini au kwa jina maarufu  “Watanzania wa kawaida”.
Panadol ya pasua kichwa hii juu ya suala la huduma za Afya ni kwa uongozi wa vyuo husika pamoja na uongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) kushilikiana kwa pamoja ili kuwasaidia wanafunzi hawa dhidi ya gharama za matibabu zinazoendela kupanda kila siku uchao  na uchwao!!
 

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA