Muhimbili Yafanikisha Upasuaji Mfumo wa Njia ya Mkojo kwa Watoto Pacha

st1
Daktari bingwa wa upasuaji wa watoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH, Dk Victor Ngotta (kushoto) akimfanyia upasuaji Eliudi jana kwa kushirikiana na Profesa Saber Waheeb (katikati) na Dk Mohamed Malak kutoka Misri (kulia).
st2
Dk Mohamed Malak, Profesa Saber Waheeb kutoka Misri na Dk Victor Ngotta wakiendelea na upasuaji jana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
st3
Daktari Bingwa Watoto wa Upasuaji, Dk Zaituni Bokhary akizungumza jambo baada ya kumfanyia upasuaji mtoto Elikana aliyekuwa na tatizo la mfumo wa njia ya mkojo jana.
st4
Dk Bingwa wa Upasuaji, Dk Yona Ringo akiwa ofisini baada ya kumfanyia upasuaji mtoto Elikana ambaye alikuwa na tatizo la mfumo wa njia ya mkojo jana.

Na John Stephen MNH
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jana imefanikisha kuwafanyia upasuaji watoto pacha ambao walikuwa wana tatizo katika njia mkojo.

Watoto hao wametoka katika chumba cha upasuaji salama na sasa wanaendelea vizuri baada ya kurejeshwa wodini. Watoto hao ni Eliudi Joel na Elikana Joel ambao wana umri wa miaka mitatu kila mmoja.

Daktari Bingwa Watoto wa Upasuaji, Dk Zaituni Bokhary na Dk Bingwa wa Upasuaji, Dk Yona Ringo wamefanikisha upasuaji wa Elikana wakati Eliudi amefanyiwa upasuaji na Profesa Saber Waheeb na Dk Mohamed Malak kutoka Misri kwa kushirikiana na Dk Victor Ngotta na Dk Mwajabu Mbaga wa Muhimbili.

Dk Bokhary amesema kuwa upasuaji wa watoto hao umechukua saa moja na nusu na kwamba hivi sasa wanaendelea vizuri baada ya shughuli hiyo.
“Watoto hawa wataendelea kuwapo wodini hadi watakapopona vizuri ndio tutawaruhusu,” amesema Dk Bokhary.

Dk Bokhary amesema kuwa watoto wengine wawili jana wamefanyiwa upasuaji ambao walikuwa na tatizo kama hilo.
Juzi madaktari wa hospitali hiyo walianza upasuaji kwa watoto wenye matatizo ya njia ya mkojo na mfumo wa hewa na chakula

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA