Shemeji wa ZARI aibula na kudai TIFFAH si mtoto wa Diamond!
Kazi ipo! Siku chache baada ya kuliona jua, mtoto wa kike ‘baby girl’ wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ aliyempata kupitia kwa mwandani wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Latifah a.k.a Princess Tiffah anazidi kuwa gumzo. TIFFAH SI WA DIAMOND? Safari hii shemeji wa Zari ambaye ni rafiki mkubwa wa aliyekuwa mumewe wa ndoa aliyezaa naye watoto watatu wa kiume, Ivan Ssemwanga aitwaye King Lawrence ameibuka na kudai: “Tiffah si mtoto wa Diamond.” Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uganda, King Lawrence, mwenye makazi yake nchini humo na Afrika Kusini ‘Sauz’ ameacha watu midomo wazi kwa kuendelea kusisitiza kuwa Tiffah ni damu ya Ivan. GUMZO UGANDA Vyombo hivyo vimeenda mbali zaidi kwa kudai kuwa Tiffah hafanani na Diamond bali Ivan, jambo lililoibua gumzo kubwa nchini humo. Hata hivyo, vyombo hivyo vilidai kuwa kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya familia ya Diamond, sura ya mtoto huyo ni Ivan mtupu kwani anafanana na wanaye watatu aliozaa na Zari. KINARA NI K