Posts

DIAMOND NA JOKATE WAMWAGANA

Image
PENZI motomoto kati ya mwanamuziki wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’ na Mrembo Nambari 3 wa Tanzania 2006, Jokate Mwegelo limedaiwa kuvunjika Kwa mujibu wa chanzo chetu, raia wa Tanzania anayecheza mpira wa kikapu nchini Marekani, Hasheem Thabit Manka anatajwa kuwa chanzo cha penzi la wawili hao kusambaratika. Awali, Thabit aliwahi kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba ‘anatoka’ na Jokate, madai ambayo kwa upande wake mrembo huyo aliyakanusha vikali akisema anasingizwa licha ya kujikanyaga katika maelezo yake. Hata hivyo, baadaye wawili hao ikasemekana wamemwagana kwa sababu ambazo hazikuwa wazi kwa vile uhusiano wao ulikuwa wa siri kubwa. Safari hii, kwa mujibu wa chanzo chetu, Hasheem amemrudia Jokate kwa nguvu zote huku ikidaiwa kwamba hitimisho la uhusiano wao litaishia kwenye kufunga ndoa na kuishi kama mke na mume. Sosi mmoja alimjulisha paparazi wetu kwa staili ya kumuuliza swali kama anafahamu lolote kuhusu wapenzi hao kupeana mkon

HIVI NDIVYO DIAMOND ALIVYOPERFORM KATIKA EVICTION PARTY YA BIG BROTHER (BBA 7)

Image
Diamond alikuwa nchini Afrika Kusini Jumapili hii kwa ajili ya performance maalum wakati wa Eviction Party ya Big Brother Africa.Hivi ndivyo ilivyokuwa performance yake BBA7

Dkt. Bilal azindua vitabu vya Yussuf R. Makamba: Binadamu na Kazi; Ukweli kwa mujibu wa Biblia, Kurani Tukufu, Suna za Mtume (SAW) na Sheria za Nchi

Image
                          Makamu wa Rais, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionesha Kitabu cha Binadamu na Kazi baada ya kukizindua kitabu hicho kilichotungwa  na Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, Yussuf Makamba (kulia) wakati ya uzinduzi uliofanyika tarehe 27 Mei 2012 kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mke wa katibu huyo, Mama January Makamba. 

HOTUBA YA NAIBU KATIBU MKUU CHADEMA,MH.ZITTO KABWE KWA WANA-CHADEMA NA WATANZANIA NCHINI MAREKANI

Image
Tumekutana leo wakati ambao Taifa letu lipo katika mpito wa mambo mengi sana. Kufuatia shinikizo kubwa kutoka chama chetu cha CHADEMA na asasi nyingine za kiraia ikiwemo viongozi wa dini, tupo katika mchakato wa kuandika upya katiba ya nchi yetu. Lakini pia kuna muamko mkubwa sana wa haki za kiraia na haki za kisiasa katika Taifa letu hivi sasa. Watanzania, kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya nchi yetu, wameamka na kutaka mabadiliko ya kisiasa na hasa kutaka kabisa uongozi mpya wa nchi kutoka chama kingine tofauti na chama kinachoongoza hivi sasa. Huu mpito pia, Mpito wa kutoka chama kimoja hodhi kwenda mfumo wa kweli wa vyama vingi vya siasa. Watanzania wameamka sana kujua rasilimali za nchi yao na kutaka kutokomeza rushwa na ufisadi na matumizi mabaya ya utajiri wa nchi. Huu ni mpito wa kutoka viongozi wanaojali maslahi yao binafsi na kwenda kwa viongozi wawajibikaji na wenye uchungu wa kuendeleza nchi yetu na watu wake. Mpito wowote unapaswa kuongo

BIFU JIPYA CYRILL NA OMMY LAIBUKA....

Image
BAADA ya msanii aliyevuma na wimbo Nai Nai Faraji Nyembo Ommy Dimpoz kumuua kwa maneno msanii Cyrill, sasa yamemrudi baada ya Cyrill naye kuongea yasiyofaa kumhusu Ommy Dimpoz. Ommy Dimpoz alinukuliwa katika kituo kimoja cha redio akisema kuwa Cyrill ni msanii ambaye hafanyi shoo kabisa. "Huyu jamaa amekosea kwa kwa kukimbilia katika vyombo vya habari na kuzungumza tu, siku nyingine ajipange kabla ya kufanya mahojiano yoyote, kwani ukiwa msanii wewe ni kioo cha jamii, haifai kuongea kila linalokuja kichwani mwako" alisema Cyrill Bifu hili jipya kati ya wasanii hawa limetokana na kuzuiwa kwa Cyrill kufanya show na BASATA siku ya Jumapili iliyopita pale Club Maisha akidaiwa hana kibali kwani ni raia wa Kenya. Ommy Dimpoz naye alikuwa na shoo yake siku hiyo Billcanas. Baadaye Ommy Dimpoz alifunguka kwenye vyombo vya habari na kusema Cyrill anatangaza kuwa yeye ndiye kamfanyia fitna ili asifanye shoo hiyo, jambo alilokanusha.

MHESHIMIWA VICK KAMATA ATOA MSAADA WA BAISKELI KWA WALEMAVU MKOA WA GEITA WILAYA YA NYAKAMWAGA

Image
Mbunge wa viti maalum CCM mkoani Geita, Mh Vick Kamata akisalimiana na mtoto ambaye ana ulemavu wa mguu kwa muda wa miaka 15 tangu sasa tangu alipozaliwa huyu ni mmoja kati ya waliokabidhiwa baiskeli ili kuwawezesha katika harakati za maisha hususani kwa kijana huyu kwenye kuisaka elimu. Victoria Foundation kwa muda mrefu sasa imekuwa ikifanya jitihada kuyawezesha makundi mbalimbali katika jamii ambapo mpaka sasa wananchi wengi katika makundi hayo yameweza kukuza vipato vyao. Kundi hili katika jamii limeweza kupata baiskeli ambazo ni imani kwamba zitafanikisha kurahisisha harakati mbalimbali za kujikwamua kiuchumi na kushiriki ujenzi wa taifa letu la Tanzania kwani walemavu wakiwezeshwa naaam wanaweza.  Baiskeli 30 zilizotolewa na Victoria Foundation kwa wananchi wenye ulemavu wilayani Nyakamwaga mkoa mpya wa Geita. Ni baadhi ya walemavu wakiwa wamepanda baiskeli zao baada ya kukabidhiwa. Ni kama fikra za ndugu zetu hawa zinasema "Sasa t

WATAKAO KISANUKISHA TAREHE 1/06/2012 NDANI YA ROCK CITY NI JAGUAR ALONG SIDE DJ ZERO

Image

RIPOTI: PICHA ZA TUKIO ZIMA LA MAANDAMANO YA WAZANZIBARI KATIKA HARAKATI ZA KUPINGA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
 Mmoja wa waandamani wa Kundi la Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI) Kisiwani Unguja,Zanzibar akionyeshan kitambaa kilicho na Damu mapema leo Asubuhi wakati wakiendelea na maandamano yao ambayo yamesababisha vurugu kubwa kisiwani humo,iliyopelekea kuchomwa moto kwa moja ya makanisa pamoja baadhi ya magari yaliyokuwa yameengeshwa karibu na njia wapitazo.vurugu hizo zimeanza jana usiku baada ya kukamatwa kwa kiongozi wa Juimuiya hiyo.  Waandamanaji wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI) wakiendelea na maandamano yao mapema leo asubuhi.  Askari wa Jeshi la Polisi kikosi cha kuzuia Ghasia wakifanya doria katika mitaa mbali mbali ya Zanzibar mapeka leo asubuhi. ***************** Baadhi ya wananchi wa Zanzibar kwenye kisiwa cha Unguja, wameandamana kupinga muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar inayopelekea kua Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Maandamano hayo yameleta mchafuko unaoendelea Zanzibar, huku ikisababisha wakazi wengi

FID Q: Nikistaafu Muziki, Ningependa kuwa kama Profes Shivji

Image
Rapper mashuhuri nchini Tanzania, Fareed Kubanda aka Fid Q amesema kama akistaafu kufanya muziki angependa kuwa Profesa kama alivyo Profesa Issa Shivji. Profesa Shivji ni mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika masuala ya sheria. Fid ambaye anajulikana sana kwa utunzi wa mashairi mazito, alikuwa akijibu swali la shabiki katika utaratibu aliojiwekea kila weekend wa kujibu maswali kupitia Twitter. Kuhusu swali lililomuuliza kama ana mpango wowote wa kujiingiza kwenye siasa kama walivyofanya wasanii wengine husasan Joseph Mbilinyi aka Sugu ambaye ni mbunge wa Mbeya mjini, Fid aka Ngosha amesema bado hana mpango huo kwa kujibu, “bado lakini juzi nilikutana na msafara wa John Mnyika nikavutiwa na zile shamrashamra!” Rapper huyo kutoka Mwanza anayejulikana kwa kuwa msomaji mzuri wa vitabu husasan vya filosofia amemtaja Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kama mwanafilosofia anayempenda zaidi katika muda wote (all time favourite philosopher). source www.freebongo.blo

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,Mh. January Makamba atembelea Airtel Tanzania

Image
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kushoto) akipokewa na Mkurugenzi Mtendai wa Airtel Tanzania,Sam Elangallor, alipofanya ziara kukagua shughuli mbalimbali za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mkurugenzi wa Mawasilino wa Airtel, Beatrice Singano Mallya. Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kushoto) akipokewa na Ofisa Mkuu wa Biashara wa Airtel Tanzania, Chiruwi Walingo alipokwenda kufanya ziara ili kukagua shughuli mbalimbali za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo.Katikati ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel,Beatrice Singano Mallya. Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice Singano Mallya akiongozana na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kushoto) katika ofisi za makamo makuu ya Airtel wakati wa ziara yake kukagua shughuli mbalimbali za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sam Elangallor (katika

MISS NYAMAGANA WAENDELEA KUTESA

Image
Shindano la Miss Nyamagana 2012, Litafanyika katika ukumbi wa Gold Crest Mwanza, tarehe 02/06/2012 ambapo wasanii Linah, Ditto na Hafsa Kazinja watalipamba jukwaa. Mc katika shindano hilo ni msanii maarufu katika tasnia ya uchekeshaji na mzungumzia Mpoki.  Jumla ya warembo 20 watapanda jukwaani kumpata Miss Nyamagana 2012, kabla ya shindano la kumpata mrembo wa Mkoa wa Mwanza. Katika mahojiano yaliyofanyika, warembo wameonekana kuwa na shauku kubwa ya ushindi, wakiaahidi kurudisha taji la Miss Tanzania Mkoani Mwanza. Shndano la Miss Nyamagana 2012 linaandaliwa na Stoppers Entainment ya jijini Mwanza.

AY akamilisha shooting ya video yake Afrika Kusini

Image
Kazi ya kushoot video ya Ambwene Yesaya aka AY iliyofanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini imemalizika salama jana. AY aliambatana na producer wa wimbo huo uliokuwa ukifanyiwa video, Marco Chali wa Mj Records. Video hiyo ambayo kwa mujibu wa AY imegharimu $20,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 30 za Tanzania, imeongozwa na director wa Nigeria anayeishi nchini Afrika Kusini Mike Ogeke wa kampuni ya GodFather Productions. Wakati wa shooting hiyo wanamuziki mapacha wa kundi la P-Square, Peter na Paul Okoye walikuwepo japo haijulikani kama wataonekana kwenye video ya AY kwakuwa nao walikuwa wakifanya video yao na kampuni hiyo. Baada ya kukamilisha shughuli hiyo AY alitweet,” I_Am_Godfather are very professional,great team EVER,we gonna shoot more videos with them.” “Had a great shoot with Tanzanian hottest artist, @AyTanzania! #its a wrap! Good working with you sir!” aliandika mmoja wa watu waliohusika kushoot video hiyo. Katika hatua nyingine AY ames