BIFU JIPYA CYRILL NA OMMY LAIBUKA....


BAADA ya msanii aliyevuma na wimbo Nai Nai Faraji Nyembo Ommy Dimpoz kumuua kwa maneno msanii Cyrill, sasa yamemrudi baada ya Cyrill naye kuongea yasiyofaa kumhusu Ommy Dimpoz.

Ommy Dimpoz alinukuliwa katika kituo kimoja cha redio akisema kuwa Cyrill ni msanii ambaye hafanyi shoo kabisa.

"Huyu jamaa amekosea kwa kwa kukimbilia katika vyombo vya habari na kuzungumza tu, siku nyingine ajipange kabla ya kufanya mahojiano yoyote, kwani ukiwa msanii wewe ni kioo cha jamii, haifai kuongea kila linalokuja kichwani mwako" alisema Cyrill
Bifu hili jipya kati ya wasanii hawa limetokana na kuzuiwa kwa Cyrill kufanya show na BASATA siku ya Jumapili iliyopita pale Club Maisha akidaiwa hana kibali kwani ni raia wa Kenya.
Ommy Dimpoz naye alikuwa na shoo yake siku hiyo Billcanas.
Baadaye Ommy Dimpoz alifunguka kwenye vyombo vya habari na kusema Cyrill anatangaza kuwa yeye ndiye kamfanyia fitna ili asifanye shoo hiyo, jambo alilokanusha.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA