Taarifa: TFDA yafanya uchunguzi, yazitaja dawa bandia zilizopo sokoni, zitambue, jihadhari
Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ni taasisi iliyo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yenye jukumu la kudhibiti usalama, ubora na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya ya jamii kwa kuzuia athari zinazoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya bidhaa hizi. Kati ya tarehe 28 Mei na 12 Juni 2012, TFDA ilifanya Operesheni Maalum katika maeneo mbalimbali Kanda ya Ziwa ikiwa ni mwendelezo wa Operesheni za kubaini bidhaa duni na bandia kwenye soko kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi nchini pamoja na Ofisi za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) za mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera. Ukaguzi na upekuzi ulifanyika kwenye maduka ya dawa, kituo cha mabasi ya kwenda mikoani, nyumba za makazi ya watu, nyumba za kulala wageni na ofisi zinazojishughulisha na kuuza shajala (stationeries). Lengo la Operesheni hii lilikuwa ni kuwabaini na kuwakamata wale wote wanaojihusisha na biashara ya dawa duni na bandia kinyume cha Sheria ya Chakula, D