BONDIA WA URUSI AINGIA MITINI, ALIKUWA APAMBANE NA RASHID MATUMLA

Mrusi wa Matumla amemkimbia baada ya kuona rekodi yake ni kali. Wawili hao walikuwa wacheze katika mpambano uliopewa jina la “The Rumble on the Mountain” na ulikuwa ushuhudiwe na mcheza sinema maarufu kutoka nchini  Marekani Deidre Lorenz ambaye atakuwa anashiriki mbio za Mount Kilimanjaro marathon mjini Moshi tarehe 24 Juni mwaka huu.
Deidre Lorenz anajulikana sana kwa sinema nyingi mojawapo zikiwa The Santorini Blue, Perfect Strangers, The Big Fight na nyingine nyingi. Hata hivyo Deidre Lorenz ataingia mjini Moshi akitokea nyumbani kwake New York , Marekani terehe 21 Juni tayari kikimbia mbio hizo za Mt. Kilimanjaro Marathon.

Bondia huyo wa Urusi Vitaly Shemetov ambaye anajulikana kama “Siberian Tiger” aliingia mitini kiaina baada ya kupelekewa tiketi za ndege ya shirika la Kirusi la Aeroflot yeye na kocha wake. Hii ni mara ya kwanza kwa mpambano wa kimataifa ulioandaliwa kwa pesa nyingi kutofanyika baada ya bondia mmojawapo kuingia mitini kwa woga.

Bondia Rashid Matumla anayejulikana kama Snake Boy ana rekodi ambayo mpaka sasa hakuna bondia yeyote wa Kitanzania aliyeweza kuifikia.

Matumla ameshawahi kuwa bingwa wa Taifa, Afrika Mashariki na Kati, Bara la Afrika, Mabara na Dunia aliyetambuliwa na Umoja wa Ngumi Duniani (WBU). Akiwa chini ja DJB Promotions bondia Rashid Matumla ambaye kwa sasa ndiye Kamishna wa TPBC kanda maalum ya Dar-Es-Salaam alionyesha ubingwa wa hali ya juu.

Hata hivyo Rashid Matumla  amepangiwa kupigana na bondia mwingine siku za usoni  ili kupooza machungu ya kukimbiwa na Mrusi huyo!

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA