Posts

KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MAMA YANGU GODRIVER POTI

Image
LEO ni miaka mitatu imepita tangu mama yangu mzazi GODRIVER POTI alipotutoka duniani,kiukweli hii ni siku ambayo huwa siwezi kuisahau maishani mwangu,kwani nilimpoteza mtu aliyekuwa muhimu sana tena sana nadiriki kusema hivyo kwa kuwa ndiye aliyekuwa msatali wambele kuhakikisha watoto wake tunapata elimu bora,tunajengeka kimaadili kwa kuturekebisha pale tulipokuwa tukikosea lakini pia akusisita kutuonyesha njia iliyosahihi ya kufuata ili kuweza kufanikiwa kimaisha. Pumzika kwa Amani mama huko uliko siku zoteza maisha yetu hapa duniani tunakukumbuka sana  na tunaamini kuwa siku moja tutaweza onana,Watoto wako Nyanja,Erick,Masatu,Jackqueline na Felister Tunakukumbuka sana tunakosa upendo wako..mama unakumbukwa na dada zako,marafiki na jamaa kwa ujumla.           Upumzike kwa amani mama

HAPPY BIRTHDAY I MA SELF

Image
rrToday is my birthday,I would like to take this opportunity to thank God for his blessing to me,there are many people who  had many dreams to reach to this beautiful day but they have passed away,am not too curious,intelligent or whatever I can say but this is because of the God love upon me!!!!!! Thanks to ma family, all my best fiends always are the good adviser to what am doing and are the one who shape me to me in this way I am,also to my fellow colleague at st.Augustine University as well as to all CRDB staff at Musoma Branch where am doing field attachment during this period of vacation. HapPy BiRtHdAY NyaNJa

HIKI NDO KINANIFANYA NISIUPTODATE BLOG

Image
Nimekuwa nikipata maswali mengi kutoka kwa wadau wa blog hii kuhusu kwa nini siku hizi blog hii imekuwa ikidorola sana kwa upande wa news,kiukweli hata mimi ninajisikia vibaya sana wadau kwakupata comments za namna hiyo..... Back to the point wadau kwa sasa niko Musoma nipo field katika bank ya CRDB hivyo nakuwa busy na kazi tangu asubuhi mpaka muda wa kutoka sa 11 jioni,nikitoka hapo nakuwa nimechoka hivyo najirudisha home kwa ajili ya mapumziko.Napenda kuwaondoa shaka wapenzi wote wa blog hii pindi muda utakapokuwa unapatikana basi nitakuwa nikijitahidi kuleta habari mbili 3 ili blog nayo isiwe dormant....

PINDA KUONGOZA MAZISHI YA MWALIMU WA MWALIMU J.K NYERERE

Image
Enzi za uhai wake marehemu Mzee James Irenge ambaye alikuwa mwalimu wa baba wa taifa Julias Kambarage Nyerere katika shule ya Msingi Mwisenge, amefariki akiwa na umri zaidi ya miaka 120 na ameacha watoto 12, wajukuu 30 na vitukuu 15. Na.  Shomari Binda: Musoma W aziri mkuu wa Tanzania Mizengo Peter Pinda amewasili Mjini Musoma mchana huu kwa ajili ya kuongoza viongozi wa Serikali katika kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Mwalimu wa Mwalimu Nyerere mzee James Irenge aliyefariki dunia nyumbani kwake maeneo ya Mwisenge katika Manispaa ya Musoma. Katika uwanja wa ndege Mjini musoma waziri pinda amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara john Tuppa,waziri wa nchi ofisi ya Rais Stevin wasira,mbuge wa jimbo la Musoma Vijijini Nimrod Mkono pamoja na viongozi wengine wa Serikali na Wananchi. Mzee Irenge, aliyekuwa na umuri wa miaka zaidi ya 120, alimfundisha Mwalimu Nyerere katika Shule ya Mwisenge, kati ya mwaka 1934

Usalama Kuimarishwa Mkoani Mara Wakati wa Zoezi la Sensa

Na Boniphace Mgendi SERIKALI mkoani Mara,imeviagiza vyombo vya dola na viongozi mbalimbali wa ngazi zote mkoani humo,kuhakikisha wanasimamia hali ya usalama kwa kuwachukulia hatua kali watu wote ambao wataonekana kukwamisha mafanikio ya zoezi la Sensa ya watu na makazi,ambalo linatarajia kufanyika nchini kote kuanzia Agosti 26 mwaka huu.   Kauli hiyo ilitolewa mjini Musoma na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Gabiriel Tupa wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya wakufunzi wa Sensa ya watu na makazi ngazi ya mkoa.   Amesema serikali haitakubali baadhi ya watu kuwa chanzo cha kukwamisha zoezi hilo muhimu kwa taifa na ambalo linatarajia kiasi kikubwa cha fedha,ambapo amesema ni wajibu wa kila kiongozi kufanya uhamasishaji kwaajili ya kuwezesha mafanikio katika zoezi hilo. Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa wa Mara,alitumia nafasi hiyo kuonya kwamba kamwe serikali hatasita kuchukua hatua kw

PUBLISH YOUR ARTICLE HERE

DO YOU HAVE AN ARTICLE?DO YOU WANT TO PUBLISH YOUR ARTICLE?DO YOU FIND THE BLOG THAT YOU CAN PUBLISH IT?THIS IS YOUR RIGHT CHOICE TO ACCOMPLISH YOUR TASK,SEND  YOUR ARTICLE TO MY EMAIL ADDRESS  kelvinnyanja@yahoo.com or kelvinnyanja@gmail.com  AND I WILL PUBLISH IT FREE OF CHARGE ,           HAVE A LOVELY WEEKEND GUYZ

HAPPY BIRTHDAY MA BRO JAILESI

Image
WISH ALL DA BEST IN YOUR LIFE,ENJOY THIS BEAUTIFUL DAY BRO.

KUMBE ABIRIA NAO WANAPENDA NJIA ZA SHORTCUT

Juzi nilikuwa natoka Shinyanga katika miangaiko ya hapa na pale,nilikuwa nimepanda basi la AM linalofanya safari zake kati ya mkoa wa Tabora na Mwanza,mimi nilipandia shinyanga kurudi Mwanza,sasa kilichonishangaza ni kwamba serikali inajitahidi kuboresha barabara zetu ili magari yaweze kupita katika barabara za lami lakini bado kuna madereva wengine hawazitumii barabara hizo na kufanya wao wanavyojua. Tulipita katika barabara ya (Old Shinyanga Road) barabara ambayo haina lami lakini pia kuna vumbi sana kiasi kwamba mwili wote ulikuwa umeogeshwa kwa vumbi la barabara hiyo,nilijaribu kuwadadisi abiria wenzangu hivi ni kwa nini dereva hatumii barabara ya lami anapita huku kwenye barabara isiyokuwa na kiwango walinijibu kuwa "Njia hii ni shortcut kuliko tukitumia barabara ya lami" nikajaribu kujiuliza maswali hivi hata abiria wao wenyewe wanapenda mambo ya shotcut na wako satisfied kabisa na jambo hili,kama mdau wa bolg hii mawazo yako ni yapi kuhusiano na jambo hili??????

17 MARA YAAHIDI USHINDI DHIDI YA MOROGORO

Na Shomari Binda, Timu ya soka ya vijana walio na umri chini ya miaka 17 ya Mkoa wa Mara leo imeahidi kuitoka timu ya vijana ya Mkoa wa Morogoro katika mchezo wa pili wa hatua ya robo fainali kwenye uwanja wa karume jijini Dar es salam. Akizungumza kwa njia ya simu na BINDA NEWS kutoka jijini humo,Meneja wa vijana wa Mara Sindbad Madenge amesema kikosi cha vijana wake wapo katika hali nzuri katika kuingia katika mchezo huo na kudai kuwa kikosi chao hakina majeruhi yeyote na wapo tayari kwa mchezo huo utakaoanza majira ya saa 10 jioni. Alisema kuwa kitendo cha kuwaondosha katika michuano hiyo mabingwa watetezi timu ya mkoa wa Kigoma kimewaongzea hali wachezaji wake lakini amewataka kutobweteka na matokeo ya mchezo huo katika hatua ya 16 bora. Katika hatua nyingine Madenge ametuma salama za rambirambi kufuatia kifo cha mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu Mkoani Mara Fabian Samo kilichotokea Julai 10 na kuiomba familia yake pamoja na wadau wote wa michezo Mkoa

POLENI KWA USUMBUFU

Poleni sana kwa usumbufu uliojitokeza kwa kipindi chote kwa wale wapenzi wa blog hii ,nilikuwa katika kipindi cha mitihani hivyo nilikuwa sipati kabisa muda wa kutosha kuweza ku uptodate information za kutosha,lakini hivi sasa msijali tena nimesharudi so more information zitakuwepo za kutosha.Pia nawashukuru sana na sana kwa kuweza kunipigia kura za kutosha mpaka kuweza kuibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha blog bora za kitanzania kwangu ni heshima kubwa sana lakini pia ni heshima kwa wapenzi wote wa blog hii kwa kuwa wamefanya chaguo halisi. Nawatakia kazi njema za kulijenga Taifa.

THE WINNER......

Image

OMMY DIMPOZ NA DJ ALLY WASHIRIKI PARTY YA KUZINDUA STONE CLUB MPYaaaaaaaa.

Image
Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini Ommy Dimpoz usiku wa kuamkia leo (nikimaanisha jana alhamisi) ameshiriki vyema kwenye party ya kuzindua Stone Club ambayo imekuja kivingine, na sevis mpya na wahudumu wapya  mara baada ya ukarabati wa muda mrefu.  Party hiyo iliyokuwa ya kimya kimya ilinogeshwa na dance la nguvu lililomwagwa na Ommy Dimpoz akishirikiana na densaz wake mahiri. Dance likiendelea katika stage ndani ya party hilo ambapo usiku huo pia ulitumika kama usiku wa kwanza mara baada ya wanavyuo kumaliza pepa. On the one and Two alisimama Dj Ally ' mzee wa kitu juu ya kitu' toka A- town ambaye alifanya makamuzi ya hatari uspime ndani ya Stone Club Mpyaaa iliyofungwa sound full kiwango ..... Dj Ally amesaini 'kontrakti'  ya muda wa kutosha hivyo ataendelea kukisanukisha hapa. Ommy Dimpoz kwa poz akicheza na shabiki wake mara baada ya mzuka kumpanda...