Usalama Kuimarishwa Mkoani Mara Wakati wa Zoezi la Sensa

Na Boniphace Mgendi
SERIKALI mkoani Mara,imeviagiza vyombo vya dola na viongozi mbalimbali wa ngazi zote mkoani humo,kuhakikisha wanasimamia hali ya usalama kwa kuwachukulia hatua kali watu wote ambao wataonekana kukwamisha mafanikio ya zoezi la Sensa ya watu na makazi,ambalo linatarajia kufanyika nchini kote kuanzia Agosti 26 mwaka huu.
 
Kauli hiyo ilitolewa mjini Musoma na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Gabiriel Tupa wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya wakufunzi wa Sensa ya watu na makazi ngazi ya mkoa.
 
Amesema serikali haitakubali baadhi ya watu kuwa chanzo cha kukwamisha zoezi hilo muhimu kwa taifa na ambalo linatarajia kiasi kikubwa cha fedha,ambapo amesema ni wajibu wa kila kiongozi kufanya uhamasishaji kwaajili ya kuwezesha mafanikio katika zoezi hilo.
Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa wa Mara,alitumia nafasi hiyo kuonya kwamba kamwe serikali hatasita kuchukua hatua kwa wakufunzi hao na kwamba haitakubali kupokea visingizio vya aina yoyote kutoka kwao baada ya kupata mafunzo hayo.
 
Kuhusu wasiwasi wa wananchi wa kupoteza muda wakati wa zoezi hilo,mkuu huyo wa mkoa wa Mara,alisema zoezi la sense halitaweza kukwamisha shughuli za wananchi kiuchumi na kwamba watoe taarifa sahihi kwa makarani bila ya hofu  kwa vile taarifa hizo mbali na kuwa za siri pia zitawezesha taifa kupanga mipango yake mbalimbali ya maendeleo.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA