SUNGU NA VINEGA WENZIE KUNUKISHA ANTI VIRUS A-TOWN

Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, ameweka kambi ndani ya A-Town pamoja na Vinega wote, wakifanya harakati za nguvu, kuwahamasisha wananchi wajae kwa wingi Uwanja wa Triple A ambako shoo kali ya Hip Hop itachukua nafasi Desemba 18, 2011 (Jumapili hii).

Sugu amesema kuwa yupo kwenye mishemishe kibao, akifanya ‘interview’ kutoka redio moja hadi nyingine za Arusha, kutengeneza uelewa kwa wana wa Arusha kuhusu harakati za Anti Virus zinavyolenga kumkomboa msanii wa Tanzania.Ni Venega wale wale wanaosababisha kizaazaa mtaani kwa mix-tape zao za Anti Virus kisha wakaibua mambo makubwa kwenye Tamasha la Burudani kwa Mashabiki, Muziki unalipa Uwanja wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama, Dar es Salaam.

Taarifa ni kwamba shoo hiyo ya Triple A, itaanza saa 8:00 mchana mpaka saa 6:00 usiku.Sugu ndiye ataongoza shoo hiyo, wakongwe Mabaga Fresh, Big Dog Pose, Hardmad, Zay B na Sister P, watafanya kieleweke..

Shujaa wa Kundi la Wagosi wa Kaya, Fred Mariki ‘Mkoloni’, Anselm Ngaiza ‘Soggy Dog’ na mwana Hot Pot Family mwenzake, Suma G, Mapacha, Dani Msimamo, Rama Dee, Peen Lawyer, Adili Mkwela ‘Hisabati’, D wa Geto, Magazijuto, Coin Moja, LWP ‘Majitu’ na wengine kibao watakuwepo kuhakikisha wana wa Arusha wanapata burudani ya ukweli ya Hip Hop.

Mratibu wa shoo hiyo, Mkoloni alisema kuwa muziki (sound) utakuwa ni wa kiwango cha juu ambao thamani yake ni shilingi milioni 50.
“Ma-DJ wenye kiwango cha juu watakuwepo kufanya mambo makubwa. Atakuwepo mtaalam,Profesa Ludigo. Wasanii watakaokuwepo ni wengi mno, tutakumbushia mapini ya kitambo na baadaye Vinega watafanya Anti Virus ieleweke,” alisema Mkoloni.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA