Posts

Shy-Rose Bhanji Amwonya Msekwa

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Shy-Rose Bhanji, amemshutumu Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa na kumtaka aache kukifanya chama hicho kama mali yake. Shy-Rose ambaye aliwania ubunge katika Jimbo Kinondoni, jijini Dar es Salaam na kushindwa kwenye kura za maoni, alitoa kauli hiyo jana akijibu kauli ya Msekwa ya juzi akiwataka wanaotaka kuhama chama hicho baada ya kushindwa kwenye uteuzi wahame haraka. Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano kwa njia ya simu, Shy-Rose alisema ameshtushwa na kauli ya Msekwa kwani hakuwa na haki ya kutamka maneno mazito na yasiyo ya kiungwana hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu. “Kwa kweli nilivyosoma gazeti moja leo nimekutana na habari hii, ikanishtua kidogo. Nikajiuliza hivi huyu mzee Msekwa anasema maneno ya ajabu namna hii, hiki chama ni chake binfasi? Pengine amejisahau kwamba CCM ni chama chetu wote, sasa iweje yeye awe na ujasiri wa kujiamini kutoa maneo ya ajabu wakati hiki ni chama chetu wote au yeye anadhani ni chama

Atakayemuonyesha Obama Matiti Yake Kulipwa Dola Milioni 1

Bilionea Alki David ili kuitangaza tovuti yake ya "Battlecam" ameahidi donge nono la dola milioni 1 kwa mwanamke yoyote atakayekuwa wa kwanza kujitokeza mbele ya rais Obama na kisha kumuonyesha matiti yake huku akiwa amebandika lebo ya "Battlecam" kwenye kifua chake. Sharti ya kushinda donge hilo nono ni kwamba tukio hilo lazima lionyeshwe LIVE kwenye tovuti ya Battlecam inayomilikiwa na bilionea huyo. Awali bilionea huyo aliahidi kutoa zawadi ya dola laki moja lakini ameamua kuiongeza zawadi hiyo iwe dola milioni 1 baada ya watu kuona dola laki moja si donge nono. "Watu wengi wanafikiria dola 100,000 hazitoshi kumfanya mtu azionyeshe sehemu zake nyeti kwenye hadhara, lakini dola milioni 1 ni pesa za kutosha kabisa", alisema bilionea Alki. Alki alisema kwamba hadi sasa jumla ya watu 150 wameishajiandikisha kuwania zawadi hiyo. Bilionea huyo alidai kuwa ameamua kumchagua Obama kwakuwa Obama ndiye kiongozi mkubwa wa dunia. Bilionea Alki alizaliwa Lagos, Nige

Tovuti za Vyama Vya Siasa nchini Tanzania

Baadhi ya vyama vya Siasa nchini Tanzania vimefungua tovuti zao ambazo huwawezesha watu mbalimbali kupata taaarifa na habari zinazohusiana chama, siasa na masuala mengine yanayoihusu nchi. Wakati tunapoelekea kwenye uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba, watu wengi walipo nje ya nchi pamoja na wafuatiliaji wa mambo wa Kimataifa wanapata taarifa nyingi kupitia kwenye mitandao, ambapo sehemu rasmi yakupata taarifa hizo ni kwenye tovuti rasmi za vyama na tume za uchaguzi. Lakini ni jambo la kushangaza na kusikitisha sana, kwamba sehemu hii ya taarifa haijapewa kipaumbele kama vile redio, televisheni na magazeti. Baadhi ya tovuti za vyama hivi hazina habari mpya tangu zianzishwe. Nyingine zina taarifa zilizochapishwa muda muda mrefu sana il hali yamekuwepo matukio mengi ambayo yangestahili kuripotiwa tangu wakati huo hadi sasa. Kwa kweli ni vigumu kung'amua ikiwa ni tatizo ni la kiteknolojia au tu kutokuipa kipaumbele TEKNOHAMA? Wahusika wa vyama na tovuti hizi tafadhalini kumbukeni kutumia to

Jay-Z Tops Hip-Hop's Cash Kings 2010 List

Image
Jay-Z needs to update his song 99 Problems , because it REALLY doesn’t seem like he has too many problems at all! At earnings of $63 million for the past 12 months, Jay-Z gets the title of #1 Hip-Hop Cash King by far. The list is based upon numbers from several music industry sources, including Nielsen, Billboard, and Pollstar. Jay-Z’s earnings derive from not only tremendous album sales, but also his earnings from his worldwide tour, the 40/40 nightclub chain, and his stake in the New Jersey Nets basketball team. Trailing far behind Jay-Z is P. Diddy , who earned the #2 spot with $30 million through album sales, television and film roles, his liquor brands, and Diddybeats ear-bud sales. Following behind Diddy is Akon at $21 million, Lil Wayne at $20 million, Ludacris at $16 million, Kanye West at $12 million, and 50 Cent at $8 million, who took a break from music work to take on film roles. While she’s not a male Hip-Hop recording artist, Jay-Z’s wife Beyonce blew absolute

mmmmmmmmmh kazi kweli kweli

Image

waliochukua fomu za kugombea urais mpaka sasa

Hadi kufikia tarehe ya leo, Jumamosi 14 Agosti 2010 wagombea waliochukua fomu za kinyang'anyiro cha Uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni hawa watuatao: 1. Richard Kiyabo - NRA 2. Jimmy Obedi Mshana - Demokrasia Makini 3. Jakaya Mrisho Kikwete - CCM 4. Peter Mziray - APPT-Maendeleo 5. Paul Kyara - SAU 6. Christopher Mtikila - DP 7. Wilbroad Slaa - CHADEMA 8. Ibrahim Lipumba - CUF 9. Mutamwega Mugahywa - TLP 10. Hashim Rungwe - NCCR-Mageuzi Kwa bahati mbaya, wasifu wa wengi wa wagombea hawa imekuwa ni vigumu kuupata habari hii ni kutoka tovuti ya www.wavuti.com

Maziwa, Chilli, Pipi na Biskuti toka TFDA ambazo zimezuiriwa

Bidhaa za vyakula kama vile maziwa chapa NAN2 na vikolombwezo vya vyakula kama vile pilipili ya chupa (chilli), peremende (pipi) na biskuti vimepigwa marufuku na mamlaka inayohusika na chakula Tanzania, TFDA, kufuatia kugundulika kuwepo bidhaa bandia na hivyo kuwa na athari na hatari kwa afya na mwili. Hatua hiyo ilitangazwa Dar es Salaam jana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, alipozungumza na waandishi wa habari. “TFDA inapenda kuutaarifu umma kuwa katika ukaguzi uliofanyika Dar es Salaam na hasa maeneo ya kuuzia vyakula, imebainika kuwepo kwa bidhaa bandia na ambazo hazijasajiliwa na Mamlaka na hivyo usalama na ubora wao kutothibitishwa,” alisema Sillo. Bidhaa zilizokamatwa ni makopo 2,261 ya maziwa bandia ya watoto wachanga aina ya NAN 2 ambayo yanatofautiana kwa kiasi kikubwa na maziwa halisi, chupa 93 za nyanya na pilipili za chupa na pakiti 149 za peremende na biskuti, ambazo hazikidhi viwango na matakwa ya sheria. Sillo alisema kutokana na ugumu wa mwananchi wa kawa

PROFESA JAY KUPAGAWISHA DALLAS LEO JUMAMOSI

Image
PROFESA JAY The heavy weight Mc, Profesa Jay Jumamosi hii anatarajia kupanda katika jukwaa la Murphy's Place Dallas nchini Marekani, baada ya 255 kumsaka Profesa Jay kwa muda mrefu bila mafanikio hatimaye leo majira ya saa sita za mchana mtu mzima akavuta wire,jamaa tayari ameshapiga show Houston Texas, Washington DC, Boston na sasa hivi yupo mjini Dallas na akiendelea na maandalizi ya Show ya Jumamosi. Aidha Prof alielezea ziara yake aliyoifanya mwezi uliopita katika makao makuu ya taasisi ya Malaria no More yaliyopo jijijini New York, prof anasema yeye kama balozi wa malaria aliweza kukutana na jopo la zima la Taasisi hiyo, na alifanya vitu vingi ambavyo alishindwa kuvitaja vyote, Prof alitumia fursa hiyo kuziasa jamii zote zinazo athirika na ugonjwa wa malaria, kwa kusema kila mtu apigane kwa uwezo wake ili kuutokomeza ugonjwa huo unao ongoza kwa kuua watu wengi nchini. Profesa alimalizia kwa kusema "Malaria haikubaliki" ukitaka kufahamu mengi tuliyozungumza na Profesa

Ufunzi wa Hasheem Thabeet kwa vijana waanza

Image
Mchezaji wa ligi kuu ya mpira wa Kikapu nchini Marekani, almaarufu, NBA, akiichezea timu ya Memphis Grizzlies, Hasheem Thabeet yupo nyumbani Tanzania kwa lengo la kuwafunza vijana mbinu sahihi za mchezo huo kupitia programu maalumu ya Basketball Clinic . Jana katika ukumbi wa ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Hasheem alizungumza na waandishi wa habari akielezea kuwa programu hiyo rasmi jana tarehe 12 Agosti 2010 kwenye viwanja vya Don Bosco. Watoto zaidi ya 400 wanatarajiwa kukutana kwenye clinic hiyo. Makamu Mwenyekiti wa shirikisho la mchezo wa kikapu nchini, Tanzania Basketball Fedreration (TBF) bw. Phares Magesa amewataka vijana wote watakaotaka kushiriki mafunzo haya kujiandikisha katika shule zao zenye vilabu vya mchezo wa basketiboli. Hasheem alisema kuwa programu hii imeshaendeshwa katika nchi kadhaa barani Afrika zikiwemo Nigeria, Senegal, Ivory Coast na sasa Tanzania. Barani Asia alishirikiana na Yao Ming kuendesha programu iyo hiyo kwenywe nchi za HongKong, Quatar

mtoto wa kitaa kutoka TMK akiwa na wakitaa mwenzie kutoka Brooklyn

miss Mara afunika miss lake zone

Image
HUYU NDIYE VODACOM MISS LAKE ZONE 2010 FATMA IBRAHIM KUTOKA MUSOMA ALIYESHINDA KATIKA KINYANG'ANYIRO KILICHOFANYIKA USIKU WA KUAMKIA LEO NDANI YA KIWANJA KIPYA KABISA HUJAWAHI TIA MGUU, NATILO HOTEL JIJINI MWANZA. KUTOKA KUSHOTO MSHINDI WA TATU VODACOM MISS LAKE ZONE 2010 BUDURI IBRAHIM NA KULIA KABISA MSHINDI WA PILI MAGRET GODSON KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MISS LAKE ZONE 2010 FATMA IBRAHIM(KATIKATI). KWA MUJIBU WA KANUNI ZA MISS TANZANIA WOTE HAWA WAMEINGIA KATIKA MCHAKATO WA FAINALI ZA KUMTAFUTA MISS TANZANIA. picha ni kwa hisana ya blog ya gsengo

USIKU WA FIESTA ULIVYOFUNIKA HAPA DAR

Image
Lil Kim baada ya kupiga songi zake kadhaa,alimuita msanii Juma Nature jukwaani na kuanza kuimba nae,ama kwa haki kuliibuka makelele na mayowe ya shangwe ile mbaya uwanjani hapa. Vijana wa kundi la Bracket toka Nigeria wakikupa 'Yori Yori' Mkali wa aladji aladji kutoka Ivory Coast,Jeff akimchezesha densa wake na kibao chake maarufu kabisa cha aladji mbele ya umati mkubwa uliofika kwenye tamasha la fiesta jipanguse. Kundi la Wanaume TMK,Chege,Temba na Kr Mulla wakilivamia jukwaani vyema kabisa na moja ya wimbo wao wa Mambo bado,Makelele yalitawala hapa uwanjani ile mbaya ni full . Ni barnaba na Lina hawa pia walipangawisha mbaya na kibao chao cha wrong no Mkali Roma on the stage,huyu jamaa nilikuwa sijawai kumuona on the stage lakini kitu nilichokiona ni kwamba jamaa ni mkali sana,watu walinyanyua mikono yao kumpa support ya kutosha. Umati wa watu uliojitokeza kwenye usiku wa fiesta Mambo ya aladji ,hawa madensa wanakata viuno ni hatari Lil kim on the stage Lil kim pia ali