Posts

Kanisa Katoliki latoa tamko kuhusu Dkt. Slaa

KANISA Katoliki limekuja juu na kukanusha tuhuma zinazoelekezwa kwa kanisa hilo kuwa limemtuma Dkt. Willibrod Slaa kuwania urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu. Vile vile kanisa hilo limesema kuwa Kanisa Katoliki si taasisi inayojihusisha na harakati za kisiasa wala si chama cha kisiasa kinachohusika kwa namna yoyote ile na uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Mhashamu Jude Ruwa'ichi alisema kuwa habari za kanisa hilo kuhusishwa na Dkt. Slaa katika harakati zake za siasa zimelenga kulichafua kanisa na kulipunguzia heshima ndani ya jamii. "Tunapenda Watanzania wenzetu waelewe kuwa Kanisa Katoliki halijamtuma wala halitamtuma mtu yeyote kugombea nafasi ya uongozi kwa jina la kanisa, kwani si jukumu lake...kanisa litaendelea kuhubiri upendo, haki, amani, mapatano na mshikamano na litaendelea kutoa mchango wake n

Mwasiti, Hussein Machozi, Lina, Adam - Bus breakdown - Fiesta 2010

Find more videos like this on TEEN TZ

Mchungaji agoma kuzika majambazi

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), amekataa kushawishika amzike Kikristo moja ya Majambazi kati ya wawili waliyouawa na Jeshi la Polisi na kukaa kwenye jokofu la Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa siku saba. Jambazi hilo linalojulikana kwa jina la Gerald Machange (26), na lenzie Paulo Yohana (18), ya Chang’ombe mkoani hapo, yaliuawa baada ya kujaribu kuwatoroka Polisi toka kwenye gari yalipokamatwa na vitu walivyokuwa wakiiba kwenye Hotel ya Emirates. Akiwafariji wafiwa na Waombolezaji nyumbani kwa wazazi wa jambazi Machange, Mchungaji Naftari Njavike wa KKKT Chinangali aliuambia umati uliofurika msibani kwamba, Neno la Mungu linatuasa kuwa, ‘Niangalieni mimi Mkaokolewe’; Lakini watu wameaacha kumuangalia Mungu na badala yake wanaangalia vitendo viovu. “Nawataka mfahamu, Kanisa halina nafasi ya kutetea tabia mbovu za namna hiyo, zinazofanywa kwenye jamii zenye lengo la kuwakosesha amani, utulivu, mshikamano, na tija ya wananchi katika maendeleo yao ya kila si

Miss Open University of Tanzania Leo

Image
Warembo washiriki wa Shindano la Miss Open University of Tanzania Excellence 2010,wakiwa wamejipanga kwa ajili ya picha.Shindano hilo linatarajia kufanyika leo katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria (Open University of Tanzania) kilichopo Kinondoni Biafra.Warembo wanaoshiriki katika shindano hilo ni Kiran Mohamed,Bahati Abdallah,Christine Justine,Veronica Allan,Salma Ally,Rehema Faraji,Zahara Muhidin,Nancy Muray,Mariana Kavishe,Jacqueline Mwombeki na Glory Mosha.FM Academia wazee wa Pamba ndio watakaopendezesha shindano hilo kwa upande wa burudani.Shindano hilo linakuja kwa udhamini wa Vodacom Tanzania,Times Fm,Clouds Fm na Mount Moriah Hotel iliyopo Kinondoni

MUSOMA KUMEKUCHA SASA

Image
Augustin Mgendi Anaitwa Augustin Mgendi ni mwana habari aliyesoma Royal jijini Dar es Salaam na sasa ni mtangazaji wa redio Victoria fm ya mjini Musoma na mwakilishi wa gazeti la Jambo Leo mjini Musoma. Umati wa wakazi wa kata ya Mkendo mjni Musoma ambao jana walijitokeza kuwasikiliza wagombea wa CCM wanaoomba ridhaa kuwakilisha bendera ya CCM katika nafasi ya ubunge katika jimbo la Musoma. Picha ya wagombea wa ccm wanaomba ridhaa ya wana CCM wenzake wa kwanza kulia ni Deus Munasa na Mbunge anayemaliza muda wake Vedastus Mathayo. Ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya ubunge katika chama cha Mapinduzi CCM ambaye amesoma Korea na sasa amerudi nyumbani kuleta mabadiliko anaitwa Eiud Esseko Tongolo ambaye ana kauli mbiu ya Changamoto ya mabadiliko Musoma (Challenge Musoma Change). Picha ya katibu wa CCM mkoani Mara akiwa ofisini anaitwa Ndekubali Ndeng'aso Habari hii na picha ni kwa hisani ya mdau Augustin Mgendi

HAPPY BIRTHDAY B-DOZEN

Image
'B-dozen' Leo ni Birthday ya Hamisi Mandi aka 'B-dozen' mtangazaji maarufu wa kipindi cha XXL cha Clouds FM,sijui unafikisha miaka mingapi lakini all in all tunakutakia maisha marefu brother.HaPpY bIrThDaY 'B-dozen'.

BBA All Star-Mwisho Mwapamba mjengoni tena

Image
Mwisho Mwapamba BBA All Star Ni habari nyingine Ilianza Big Brother Africa mwaka 2003, ikaja Big Brother Afrika II (2007), ikaja Big Brother III (2008), baadaye Big Brother Revolution (2209), hata hivyo, zote zinatajwa ni tisa, 10 na itakayofunika ni ya 2010 ambayo inakwenda kwa jina la Big Brother All Stars. Sababu ambayo inatajwa kuifanya Big Brother mwaka huu kuwa ya kipekee ni uamuzi wa kuwachukua mastaa waliong’ara kwenye fainali zilizopita na kuwapa nafasi ya kuingia tena mjengoni ili kushindana tena. Tanzania imeshiriki mashindano hayo mara zote, na kufanya vizuri zaidi mwaka 2007, pale Ricahrd Bezuidenhout aliponyakua taji na kujibebea kitita cha Dola za Kimarekani 100 ambazo kwa ‘chenji’ ya wakati huo zilikuwa shilingi 130,000,000. Mwanga wa mafanikio kwa Tanzania kwenye mashindano hayo, ulioneshwa mapema mwaka 2003, pale Mwisho Mwampamba ‘Mr. Morogoro’ aliposhika nafafasi ya pili, nyuma ya Cheris Makubale wa Zambia. Mwaka 2008, Tanzania iliwakilishwa na Latoya Lyakurwa ambaye

MAMIA WAJITOKEZA KUMSIDIKIZA VINCENT NYERERE KURUDISHA FOMU

Image
Vincent Nyerere pamoja na Kambarage na wananchi wa jimbo la musoma mjini Wakazi wa jimbo la Musoma mjini leo wamejitokeza kwa wingi wakimsidikiza mgombea Ubunge wa jimbo la Musoma mjini kwa tiketi ya chama cha CHADEMA bwana Vincent Nyerere wakati wa urejeshaji wa fomu ya kugombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho.wadau wote wa blog hii wanakutakia kila la kheri katika kuuletea mkoa wetu Maendeleo.

Manchester United Kits 2010/2011

Image
Manchester new jersey Share all new kit debates/images in here. Before I start, you should realise that I am not claiming these to be real or official, but have found them on the internet in various places, and as you might expect, there has been much discussion!

BIG BROTHER AFRICA 2010 KUANZA KESHO

Image
Lile shindano maarufu la Big Brother Africa kwa mwaka huu wa 2010 linatarajiwa kuanza rasmi Jumapili kesho tarehe 18 Julai 2010 huko Johanesburg nchini Afrika Kusini. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kampuni ya MultiChoice Tanzania , jumla ya washiriki 14 watatambulishwa siku hiyo wakati wakiingia katika Jumba la Big Brother. Shindano hilo litadumu kwa siku 91. Mshindi wa Big Brother 2010 anatarajiwa kuondoka na kitita cha US Dollars 200,000. Kama kawaida shindano hilo litakuwa likirushwa hewani kupitia kituo cha DStv-Channel 198. Tangu shindano hilo lianzishwe,kumekuwa na maoni tofauti tofauti kuhusu faida au hasara za shindano kama hilo.Wapo watu ambao wamekuwa wakidai kwamba shindano hilo linachangia katika kuporomoka kwa maadili kutokana na vitendo vya ki-ngono ngono vinavyofanywa na washiriki wa shindano hilo. Pamoja na hayo,shindano hilo limekuwa likijipatia mashabiki na wafuasi chungu mbovu kila mwaka. Mwaka jana Tanzania iliwakilishwa na mmoja wa wash

Ni Robo Tu Ya Wanaume Wa Dar Wenye Mbegu Zenye Rutuba

IMEFAHAMIKA, kuwa idadi ya wanaume wa Kitanzania wenye mbegu za uzazi zisizorutubisha hivyo kutoweza kurutubisha yai la mwanamke na kusababisha mimba inaongezeka. Kwa mujibu wa gazeti la ‘ The Citizen’ toleo la Jumamosi ( Leo), Julai 17,2010 zaidi ya asilimia 35 ya wanaume wanaofanya vipimo vya rutuba za mbegu za uzazi wamegundulika kuwa hawana. Mara nyingi lawama za kukosa mtoto katika familia zimekuwa zikielekezwa kwa mwanammke kutokana na .... Soma zaidi ; http:// www.kwanzajamii.com

NHC waanza kuwatimua Wapangaji batili

Image
Shirika la Nyumba ya Taifa (NHC) limeanza kuwaondoa kwa nguvu baadhi ya wapangaji ambao wamebainika kuishi kwenye nyumba hizo kwa kurithishana badala ya kufuata utaratibu maalumu uliopangwa na shirika. Picture Hatua hiyo imewakumba baadhi ya wapangaji katika maghorofa ya Keko Mtaa wa Magurumbasi A ambapo kazi hiyo ilisimamiwa na viongozi wa NHC na Kampuni ya udalali ya Msolopa. Mwandishi wa gazeti la DarLeo alishuhudia mpangaji Pantalelo Mushi akiondolewa vitu vyake ndani ya nyumba chini ya usimamizi wa wajumbe wa nyumba kumi. Ofisa wa NHC, Anneth Natai, amesema kumekuwa na mazoea ya wapangaji kuwarithisha watu wengine bila ya idhini ya uongozi. Kutokana na kitendo hicho, NHC imekuwa ikipatwa na usumbufu pindi kunapotokea tatizo na hata wengine kushindwa kufuata masharti yao. “Kuna wapangaji wengine wamekuwa wakilipa kodi kubwa kwa kuwapa wamiliki halali ambayo hata sisi hatuijui na pia tumekuwa hatuwafahamu wapangaji halisi,” amesema. Amesema kazi ya uondoaji wapangaji wasiotamb