SOMA HOTUBA YA RAIS WA SAUTSO MH.MALISA ALIYOITOA WAKATI WA KUVUNJA BUNGE NA SERIKALI YA WANAFUNZI


St. Augustine University of Tanzania Students’ Organisation





President Office,  C/o St. Augustine University of Tanzania (SAUT), P.O. Box 307,
Malimbe Campus, Nyegezi – Mwanza Region
WEBSITE: www.sautsolink.blogspot.com

HOTUBA YA RAIS WA SAUTSO 2012/13 ALIYOITOA WAKATI WA KUVUNJA BUNGE NA SERIKALI YA WANAFUNZI TAR.16/03/2013.

Mhe.Spika,
Mlezi wa wanafunzi,
Makamu Mkuu wa chuo Fedha na Utawala,
Mawaziri na wabunge, Itifaki imezingatiwa.
Awali ya yote natoa shukrani za dhati kwa wanafunzi, wafanyakazi na utawala wa Chuo hiki kwa ushirikiano mkubwa mlionipatia kwa kipindi changu cha mwaka mmoja wa uongozi. Nimejifunza mengi ndani na nje ya nchi. Hakuna uongozi usio na changamoto lakini ukimtumainia Mungu atakushindia yote.
Pili  nilishukuru bunge lako tukufu, mawaziri na viongozi kutoka utawala, waandishi wa habari na wadau wengine  kwa kujitokeza kwa wingi kuja kunisikiliza nikihutubia Bunge kwa mara ya mwisho kabla sijalivuja rasmi, kama nilivyopewa mamlaka hiyo na Katiba ya SAUTSO Ibara ya 9.3.3 na Ibara ya 9.6.6 kwa pamoja.

Mhe.Spika,
Serikali ya wanafuzi katika chuo kikuu cha Mt.Augustino 2012/2013 ilichaguliwa ta.25/04/2012 kwa ushindi wa 70.1% dhidi ya 29.9% alizopata mpinzani wetu katika uchaguzi uliofanyika kwa amani na utulivu lakini uliogubikwa na changamoto nyingi. Huu ulikuwa ni ushindi mkubwa kuwahi kutokea katika historia ya uchaguzi ya chuo hiki. Ushindi huu ulitoa tafsiri ya Imani kubwa ya wanafunzi wa SAUT kwetu na kukubalika kwa sera zetu kwao kupitia Ilani yetu ya uchaguzi.

Mhe.Spika,
Wakati tunaomba ridhaa ya kuongoza Jumuiya ya wanafunzi wa chuo hiki tulikuwa na Ilani ya uchaguzi yenye vipaumbele 11. Tuna furahi kuwa muda wetu wa kuwepo madarakani umekwisha nasi tunajivunia mafanikio ya 90% katika utekelezaji wa Ilani yetu ya uchaguzi. Hiyo ni level ya juu sana ktk political achievement.

Mhe.Spika,
Vipaumbele tulivyoainisha kwenye Ilani yetu japo kwa kuvitaja ni kama ifuatavyo. Kwanza ni kuhakikisha miundombinu ya kujisoea nje ya madarasa inaboreshwa, Kupata ofisi mpya ya SAUTSO, Kuimarisha Ulinzi na Usalama kwa wanachuo wote hasa wanaoishi Off-Campus, Kuboresha miundombinu ya kujisomea madarasani kama Projectors na Sound System, Kuhakikisha umeme wa uhakika kwenye maktaba ya chuo, Kuzuia mfumuko wa bei za vyakula chuoni, Kuboresha sekta ya michezo, Kuhakikisha gharama za bei za hostel za nje zinapungua, kuboresha sekta ya Afya na mwisho ni kufanikisha ununuzi wa basi la chuo.

 Mhe.Spika,
Tumefanikiwa kurekebisha sound system za madarasani na projectors. naamini mmejionea wenyewe kazi iliyofanyika na hakuna darasa linasumbua.
Tuliahidi umeme wa uhakika Library, na nimepambana sana kwny vikao vya maamuzi ndani ya chuo ikiwemo,
  •  University senate
  •  University management Board, kupeleka hoja ya kuhakikisha inatengwa bajeti ya kutekeleza hilo. Jitihada hizo zikazaa matunda na tayari zimenunuliwa solar panels zaidi ya 70 na zimeanza kufungwa ili library iwe na reliable source of energy. Nafarijika kwamba sasa wanafunzi wakiwa Library umeme ukakatika hawatafukuzwa tena kama ilivyokuwa awali.

Mhe.Spika,
Tuliomba Serikali ya wanafunzi (SAUTSO) kupata ofisi mpya baada ya ofisi inayotumika sasa kutokukidhi mahitaji ya shughuli za serikali za siku kwa siku. Nafurahi kulijulisha bunge lako tukufu na umma wa SAUT kwa ujumla kuwa  tumepata ofisi mpya opposite na  Mwanjonde Lecture Theatre.
Tayari tumeikarabati kwa kuboresha system ya choo, kuweka milango, na kuvunja baadhi ya kuta ili ionekane ofisi badala ya nyumba ya kuishi. Tumeweka mashelf. Kwa kifupi ukarabati ndani umemalizika hadi rangi, bado nje.

Japokuwa ofisi imeshindwa kukamilika kwenye uongozi wetu lakini nafarijika kuwa serikali ijayo itakuwa na ofisi mpya ambayo ni matunda ya juhudi zetu. Ofisi hii ina vyumba 6 na ile ya zamani ina vyumba 3, hivyo kwa ujumla SAUTSO itakuwa na vyumba 9 vya ofisi na kuwa Serikali pekee ya wanafunzi yenye ofisi nyingi zaidi Tanzania.

Mhe.Spika,
Tuliahidi kuboresha mazingira ya kusomea nje ya madarasa. Tulijitahidi kutafuta ufadhili ndani na nje ya chuo na hatimaye tukafanikiwa kukutana na shirika maendeleo la ujerumani ambao wameingia ubia (patnership na TiGo) katika kutusaidia.
 As the result wamekubali kutujengea vimbweta vya kusomea vya kisasa na kuboresha vilivyopo, kuanzia eneo la ATM hadi karibu madarasa ya M10 na M9. Huu ni ufadhili mkubwa maana mradi huu utagharimu jumla ya sh. Mil.79. Tayari mradi umepata baraka za Makamu Mkuu wa chuo fedha na utawala ambaye ameshasaini mkataba wa kuwaruhusu kuanza kazi.
Pamoja na pongezi kubwa tulizozipata kwa Vice Chancelor kutokana na jitihada zetu, tunaiasa serikali ijayo itoe ushirikiano wa kutosha kuhakikisha mradi huu unaanza kutekelezwa. kumbukeni mkilalala wanaweza kuona hamna nia hivyo hivyo wakakata tamaa.



Mhe.Spika,
Tumepigania wanafunzi 16 waliofukuzwa chuo kurudishwa masomoni baada ya kutetea rufaa zao kwenye Board of Appeal. Mmojawapo ni mwenyekiti mstaafu wa chama cha wanafunzi wanaosoma Kiswahili (CHAWAKAMA).Pia tulijitahidi kuwaombea msamaha wanafunzi zaidi ya 260 wa Public Relations ambao management ilishauri wafukuzwe kutokana na kufanya fujo kwenye chumba cha mtihani. We pled for clemency na wote wakasamehewa.

Mhe.Spika,
Tuliahidi kupunguza gharama za uendeshaji wa serikali ya wanafunzi (SAUTSO) kwa kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Na tumefanikiwa kupunguza matumizi ya SAUTSO kutoka mil.240 za serikali iliyopita kufikia mil.136 kwa serikali yetu. Nilishukuru bunge lako kwa kukubali mabadiliko hayo na kuipitisha bajeti yetu kwa 99% ya kura zote zilizopigwa.

Mhe.Spika,

Tumeratibu kwa ufanisi safari ya Rwanda kwa washindi wa Fawasco mwaka jana. Pia tulifanikiwa kupeleka timu nne (4) kwenye SUSAUT Gathering ya Morogoro. Awali zilikuwa zikienda timu (2) tu, yaani football na netball. Lakini chini ya uongozi wetu tumefanikiwa kuongeza timu ya Basketball ambayo ilichukua ubingwa kwa kuvifunga vyuo vingine zaidi ya 10 vilivyoshiriki. Timu yetu ya Basket ndio timu pekee ambayo haikuwahi kupoteza mchezo wowote tangu mwanzo hadi mwisho wa mashindano. Laiti tusingeipeleka ushindi huo tusingeupata.
 Pia timu ya Volleyball ambao nao tuliwapeleka wakashiriki kwa mara ya kwanza, waliingia fainali na kuibuka washindi wa pili.


Mhe.Spika,
Tumeandaa makongamano, semina, na midahalo mbalimbali yenye manufaa kwa wanachuo kama ifuatavyo:
 -Kongamano katiba ambapo tulimwalika Deus Kibamba (m/kiti Jukwaa la Katiba), Bw.Jimmy Luhende mkurugenzi wa asasi ya ADLG na wageni wengine (08/12/2012).
 -Kongamano la kujadili maadili ya taaluma ya ualimu ambapo tulikuwa na Rais wa chama cha waalimu Adrian Mkoba (05/01/2013).
-forum ya siku ya siku ya wanawake duniani ambapo tulimwalika Prof.Anne Tibaijuka lakini kwa bahati mbaya akashindwa kufika (23/02/2013).
 -Na wakati wa kuvunja bunge jumamosi ya tarehe 16/03/2013 tulihitimisha na forum ya uchumi ambapo tulikuwa na Mh.Tundu Lissu na mkurugenzi wa TPDC Bw, Yona Killagane aliyekuja kwa niaba ya waziri wa nishati na madini Prof.Sospeter Muhongo.
 Forum zote hizi zimesaidia sana kuongeza upeo wa wanafunzi wetu ktk mambo mbalimbali na kupata fursa ya kuuliza yale yaliyokuwa yakiwatatiza.

Mhe.Spika,
Tumefanikiwa kuboresha mashindano ya FAWASCO kwa kutafuta udhamini NMB na TiGo.
 NMB wametoa jezi, mipira, usafiri wa timu kwenda kambini. In advance pia watatoa flat screen mbili za inch 52 kwa SAUTSO ijayo. Tayari tumeshasign mkataba ndio maana uwanja wa Raila Odinga unashine kwa flies za NMB.
Hizo ni juhudi zetu kama Serikali yetu inayoondoka madarakani. Awali mimi na wizara yangu ya michezo tulikutana na Mkurugenz wa NMB Lake zone Mr.Straton Chilongola na baadae tukakutana na Mkurugenzi wa Masoko NMB taifa Mr.Imani Kajula katika kutekeleza azma hiyo.
In return NMB tumekubali wafungue ATM yao hapa chuoni ili kutengeneza two ways symmetrical communications kati yao na jumuiya ya chuo hiki kupitia Corporate Social Responsibility. Natumaini mmeiona ATM hiyo na kwa wateja wa NMB anzeni kuitumia kwa ari, nguvu na kasi zaidi.

Mhe.Spika,
Tunafarijika kuona ATM ya NMB iliyotokana na juhudi zetu, lakini tunafarijika zaidi kuona wachezaji wetu wakiwa wanapendeza kwny jezi za NMB.
Kwa upande wao TiGo wao watachangia Mil.6 kufanikisha Fawasco ya mwaka huu na tayari wamekabidhi kwa utawala (mbele ya DVCAF) vifaa vyenye thamani ya mil.3.5. Tigo pia watafanya tamasha kubwa siku ya fainali ambapo wamedai kumleta msanii wa kimataifa (watamtaja badae)

Mhe.Spika,
 Kwa ujumla ufadhili wa Tigo na NMB utakagharimu takribani mil.15. Haya ni mafanikio makubwa sana kwetu, kwa management na kwa wanafunzi wote kwa ujumla. Hakuna serikali iliyowahi kufanya hivi. Wakati wengine walikuwa wanaomba fedha management, sisi tumetafuta fedha kwa asasi za nje na kuzileta management. Hizi juhudi zinazopaswa kupongezwa na kila mpenda maendeleo.

 Mhe.Spika,
Tumehakikisha fedha za meals & Accommodation zinafika kwa wakati, (unless kwa wale wachache waliokuwa na special case). Pia hii ni serikali pekee ambayo imehakikisha fedha za Research zinafika kwa muda muafaka (kabla wanafunzi hawajafanya mitihani yao ya mwisho).

Mhe.Spika,
Tuliahidi bei ya chakula itabaki kuwa 1200 kwa 1500 na tumehakikisha hilo limetekelezwa. Kuna kipindi wazabuni walipandisha bei kinyemela kufikia sh.2000 kinyume na mikataba yao ya zabuni kwa kulalamikia cost of production. Lakini tuliunda kamati maalum iliyofanya uchunguzi wa kina juu ya madai hayo na kubaini kuwa madai hayo hayakuwa na ukweli wowote.
 Hivyo tukalazimika kutoa notice ya saa 24 kwa wazabuni kurudisha bei ya kawaida .(1200 kwa 1500). Tunawashukuru kwa kutii agizo hilo na kurudisha bei ya kawaida kama ilivyoelekezwa ktk mikataba yao. Yamkini tuliibua migogoro na baadhi ya wazabuni (hatuna budi kuomba radhi) lkn nia yetu ilikuwa kulinda haki za waliotuchagua.

Mh.Spika,
Tuliahidi pia kuwa na nembo (logo) yetu kama serikali ya wanafunzi badala ya kutegemea logo ya utawala ili kuweza kuwa na corporate identity yetu. Nafurahi kulijulisha bunge lako tukufu kuwa tumefanikiwa kutengeneza logo ya SAUTSO tangu mwezi August mwaka jana (2012) baada ya nembo hiyo kudhbitishwa na utawala.

Mhe.Spika,
Nembo hii sio tu kuwa itatumika katika shughuli mbalimbali za serikali ya wanafunzi, bali itabaki kuwa alama ya kumbukumbu kwa serikali yoyote itakangoza SAUTSO baada yetu, hatakama ni baada ya miaka elfu moja. Pongezi kwa wizara ya Habari na mawasiliano kwa juhudi kubwa walizozifanya kufanikisha swala hili.

Mhe.Spika,
Kwa kifupi tumefanya mengi sana, japo hatuwezi kueleza kila moja lakini tumejitahidi kadri ya uwezo wetu kutimiza yale tuliyoahidi. Kama kuna ambayo tumeacha tunaamini watakaokuja nao watafanya kwa nafasi yao.

Mhe.Spika,
Nitumie pia fursa hii kuipongeza Tume ya uchaguzi iliyoundwa jumamosi na kuapishwa juzi na mwanasheria mkuu wa chuo. Nimpongeze Mh.Lumuli Makala kwa kuchaguliwa M/kiti wa Tume. Naamini yeye na jahazi lake wataongoza tume ktk kufanya uchaguzi huru na haki na kumpata Rais ambaye ni chaguo la wana-SAUT.
Nitoe shukrani za pekee kwa baraza langu la mawaziri ambalo kila mmoja amepigana kiume kuhakikisha anawatumikia kwa ufanisi watu wa SAUT.
Nimshukuru Makamu wangu Consolatha Michael, Waziri Mkuu Baraka Mnkeni na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Nice Mberesero kwa kunishauri kwa busara ktk kipindi chote cha uongozi wangu.

Mhe.Spika,
Nikushukuru pia wewe Spika wa Bunge la SAUTSO (Mh.Lutehanga Eric) kwa kuongoza bunge kwa hekima na kuhakikisha bunge linatimiza kazi yake ya kuisimamia serikali.
Zaidi ya yote nimshukuru Makamu Mkuu wa chuo Rev.Dr.Charles Kitima kwa ushirikiano mkubwa kwa SAUTSO. Kila ninapomuona naona matumaini hata kama kuna kiza mbele yangu. Nimshukuru pia kwa kutusaidia kufanikisha safari ya SAUTSO Zambia, Malawi Rwanda na kwingineko. Mungu ambariki sana na ampe maisha marefu na yenye Baraka.

Mhe.Spika,
Niushukuru uongozi wote wa chuo kwa ujumla wake, kwa kuanzia na Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma, Makamu Mkuu wa Chuo Fedha na Utawala, Mwanasheria Mkuu wa Chuo na Mlezi wa Wanafunzi (Dean of students) kwa kutusaidia kila tulipokwama. Hawakuchoka tulipohitaji msaada wao. Tunashauri serikali ijayo iwatumie kwa ufanisi maana ni hazina ya maarifa na hekima.

Mhe.Spika,
Kwa moyo wa dhati niwashukuru waalimu wangu walioniwezesha kufika hapa, na hata nilipokuwa kiongozi hawakuniacha bali walizidi kunishika mkono na kuniongoza pale nilipoteleza. Nimshukuru kipekee Mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya Umma Madam Duwe kwa kunishauri, kunionya na kunielekeza bila kuchoka.
 Nitakuwa mchoyo wa fadhila bila kuwashukuru wanadarasa wenzangu wa B.A in Mass communications (mwaka wa tatu) kwa ushirikiano mkubwa walioonesha tangu wakati wa kampeni hadi sasa. Hawakuchoka kunishauri, kunionya nilipokosea, kunielekeza. Hata nilipozidiwa na majukumu na kushindwa kufika darasani bado walijitoa kunisaidia.  Pia shukrani hizi ziwafikie wanafunzi wote wa SAUT.
Wa mwisho japo ni wa kwanza kwa umuhimu ni wazazi wangu Mr&Mrs Malisa Joseph Elisante.

Mhe.Spika,
Zaidi ya wote nimshukuru Mwenyezi Mungu wa mbinguni kuniumba na kuwa nami ktk kila hatua ya maisha yangu,
 Leo mimi ni Kiongozi wa SAUTSO, kiongozi wa shirikisho la vyuo vikuu vya SAUT na kiongozi wa shirikisho la wanafunzi vyuo vikuu Afrika Mashariki (EACSU) kwa uweza wako Mungu. Wewe ndiwe ujuaje nitokako na ninakoelekea, uniongoze kuzifikia ndoto zangu. Wewe husema iwe ikawa, sifa na utukufu vikurudie (Zaburi 8:1-8).

 WITO KWA SERIKALI IJAYO.

Uongozi ni kujitoa sadaka, uongozi ni kujinyima, Uongozi wa kweli ni mzigo. Kuna wakati utalazimika kuacha jambo hata kama unalipenda kwa sababu wewe ni kiongozi, na kuna wakati utalazimika kufanya jambo hata kama hupendi ili kuwatumikia watu.
Ukiwa kiongozi utapoteza masomo, utakosa muda wa kufanya mambo yako binafsi, utakosa quiz, assignment kwa ajili ya kuwatumikia watu. GPA yako itatetereka kwa ajili ya utumishi uliotukuka. Kuna wakati utatumia hadi fedha zako binafsi ili mambo yasikwame, kuna wakati utakosa hata muda wa kula, muda wa kulala, pengine hata muda wa kujisomea lakini ni wachache sana watakaoappreciate juhudi zako.
Usife moyo, usikate tamaa, songa mbele ukimwomba Mungu. Wapo watakaokudisappoint kwa kukosa fursa may be ya uwaziri na kudiscredit kila unalofanya lakini usikate tamaa.
Unaweza kukosa muda wa kufanya jambo lolote binafsi. Muda wa kula, muda wa kuwajulia hali ndugu zako (wengine kwa kutokujua watasema unaringa baada ya kuwa kiongozi), unaweza kukosa hata muda wa kulala, lakini jitahidi usikose muda wa kufanya mambo mawili makubwa:Muda wa kusali na Muda wa kufanya kilichokuleta chuoni (kusoma). Hata kama utapata muda kidogo, utumie vizuri.

Mhe.Spika,
Baada ya kusema hayo natangaza kuwa kwa mamlaka niliyopewa na Katiba ya SAUTSO nimelivunja rasmi bunge la serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Mt.Augustino mwaka 2012/2013, tayari kwa mchakato wa uchaguzi.
NAWATAKIA UCHAGUZI HURU, HAKI NA WENYE AMANI. MUNGU AWABARIKI WOTE.

Malisa Godlisten
Rais SAUTSO 2012/2013.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA