Majina ya vyuo 9 vilivyofutwa na Serikali kwa kukosa sifa.

Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi  imevifuta vyuo ambavyo havina sifa ikiwamo kukosa usajili wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) na kufundishwa na walimu wasio na sifa.  Vyuo vilivyotangazwa kufutwa ni:-

1.Media and Values Training Institute(Dar es Salaam)

2.Information Technology Training Center(Dar es Salaam)

3.Dar es Salaam School of Hair Design (Dar es Salaam)

4.Morogoro School of Medical Sciences (Morogoro)

5.Media and Research Center

6.Vision Hotel and Tourism College

7.East Africa College of Hospitality and Tourism

8.The Africa Institute of Business Management

9.Aspiration Training Center


Naibu Waziri wa Wizara husika , Philip Mulugo, alitangaza hatua hiyo wakati alipokutana na Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa Sifuni Mchome, alisema Serikali ilishatangaza kuwa vyuo visivyo na sifa vifungwe lakini tatizo likawa ni jinsi ya kuwatafutia wanafunzi waliopo vyuo vingine

Source: wavuti

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA