Posts

Image
Jengo likiwaka moto. JENGO la ghorofa tatu lililopo Manzese-Bakhresa jijini Dar es Salaam ambalo linatumiwa kwa shughuli za utengenezaji wa soli za viatu na lina maduka, jana lilishika moto baada ya kutokea hitilafu ya umeme ambapo vitu kadhaa vilivyokuwemo ndani yake viliteketea. Walioshuhudia moto huo ulioanza kuwaka majira ya saa saba za mchana walivilaumu vikosi vya uokoaji na zimamoto ambavyo vilichukua zaidi ya saa moja tangu moto huo uanze kuteketeza vitu katika jengo hilo. Wafanyakazi wa Tanesco wakiondoka eneo la tukio baada ya kuhakikisha umeme hauleti tena madhara eneo hilo. Mashuhuda wakishangalia tukio hilo. Gari la polisi likiwasili eneo la tukio kulinda usalama. Gari la zimamoto la kampuni ya Ultimate Security likielekea eneo la tukio. picha hizi ni kutoka tovuti y a http:// www.globalpublishers.com

Geneviev Emanuel miss tanzania 2010

Image
Geneviev Emanuel akikabidhiwa rasmi usiku wa kuamkia leo gari yake aina ya Hyundai i10 lenye thamani ya shilingi milioni 12 pamoja na kitita cha shilingi Mil 10.watoa burudani walikuwa ni Mh Temba na Chege kutoka TMK Family, Ambwene Yessaya (AY) Mataluma, Mwasiti na kundi la THT.

SO SORRY

Samahani sana kwa wapenzi wa blog hii nilipata tatizo kidogo kwenye Internet yangu nikashidwa kupost taarifa mbalimbali katika blog yetu,lakini nimerudi tena ulingoni kama kawaida.

HAPPY BIRTHDAY 'J-RYDER

Image
'Jeremy J-Ryder Kyejo's Producer mkali toka Tongwe Records Jeremy aka J-RYDER leo anasherehekea siku yake ya kuzaliwa,wish all da best Bro on this special day

ME AND JAILES TUKICHIACHIA PANDE ZETU

Image
Kelvin nikjiachia pande fulani Me and Jailes chilin out this weekend

JAILES AKI SHOW LOVE KWENYE BLOG PIA

Image
Anapenda kuitwa JAY akishow love kwenye blog yako kama kawa ...tufurahi pamoja.

POZI LA WEEKEND

Image
POZI LA WEEKEND KAMA KAWAIDA

SHOW LOVE

Image
call him Robert Latonga aka 6 more base,aka Big R the real hommy boy akishow love kwenye blog ya lets Enjoy Together...kama kawa Big R akiwa pande za urafiki na wana wakibadilishana mawazo

REDDS FASHION SHOW

Image
Meneja wa kinywaji cha Redds kinachozalishwa na kampuni ya (TBL) Kabula Nshimo akikaribisha wageni mbalimbali walioalikwa katika onesho hilo lililoandaliwa na kampuni hiyo kama wadhamini wenza wa Vodacom Miss Tanzania linalofanyika kwenye ufukwe wa Mbalamwezi usiku huu, Shindano la Vodacom Miss Tanzania limepangwa kufanyika Septemba 11 mwaka huu jijini Dar es salaam. Mrembo Geneviva Emmanuel akipita na kivazi cha Redds wakati wa onesho la Redds fashion Show lililofanyika kwenye ufukwe wa Mbalamwezi usiku wa jana likishirikisha warembo wanaoshiriki katika shindano la Vodacom Miss Tanzania ambalo linatarajiwa kufanyika Septemba 11 jijini Dar es salaam. Warembo kutoka kanda ya Temeke wakipita na kivazi cha Redds. Warembo kutoka kanda ya kati ya wakipita na kivazo cha Redds. Warembo kutoka kanda ya Ilala wakipita jukwaani na kivazi cha Redds. Mashabiki mbalimbali wapo wakishuhudia onesho la Redds Fashion Show kwenye ufukwe wa Mbalamwezi. Mrembo anayemaliza muda wake Miriam Gerald wa pili

TIGO KUJENGA MINARA 8 MUSOMA VIJIJINI NA SERENGETI

Image
Kampuni ya simu ya Tigo inajiandaa kuanza ujenzi wa minara 8 itakayojengwa maeneo mbalimbali ya Musoma vijijini maeneo ya Suguti,Makojo,na Saragana kwa upande wa Serengeti ni maeneo ya Ngoreme,Isenye na Nyichoka hayo yamesemwa na Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo , Dallon Kango dhumuni kubwa la kujenga minara hiyo ni kusogeza huduma zao katika maeneo hayo ,aliendelea kusema kuwa "tumeamua kujenga minara hiyo kwa sababu kwa muda mrefu sasa watu wa maeneo haya wamekuwa wakiangaika kupata huduma zetu ambazo ni nafuu sana hapa nchini ukilinganisha na mitandao mingine ya simu.

THT,AY,WAHU KUPAMBA MISS TANZANIA

Image
Wasanii wa kundi la Tanzania Houde Of Talent (THT) wanaotamba na jimbo mbalimbali hapa nchini na Wahu kutoka Kenya wanatarajiwa kupamba shindano la Miss Tanzania linalotarajiwa kufanyika tarehe Septemba 11 kwenye ukumbi wa Mlimani City. Mratibu wa shindano Hashim Ludenga alisema kuwa mbali na wasanii hao,pia kutakuwa na burudani kutoka kwa AY,Mheshimiwa Temba,Chege na Mataluma. Shindano hilo linawashirikisha warembo 30 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania.

UPENDO NKONE AJIANDAA KUFUNGA NDOA

Image
Mwimbaji mashuhuri wa nyimbo za INJILI Bi Upendo Nkone ambaye amekuwa mjane kwa muda wa miaka tisa anatarajia kufunga ndoa na Mchungaji John Mbeyela oktoba 17 mwaka huu.Upendo Nkone anatarajia kuagwa oktoba 11 nyumbani kwao Kigoma,Tanzania na ndoa yake na mchungaji huyo ambaye ni mjane mwenye watoto watatu itafungwa katika kanisa la Naioth maarufu lililopo Mabibo Makuburi jijini Dar es salaam.Mwimbaji huyo aliyeanza kuimba miaka mitano iliyopita amefanikiwa kutoa albamu tatu ambazo ni Mungu Baba,Hapa Nilipo na Zipo faida .

PRECISION AIR YAONGEZA NDEGE MPYA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh.Mohammed Babu akikata utepe kama ishara ya kuzindua ndege mpya ya Precision ART 42- 500 yenye uwezo wa kubeba abiria 48 ambayo itafanya safari zake kati ya Dar es salaam na Bukoba na kurudi Dar es salaam, ndege hiyo iliruka kutoka Dar es salaam kwenda Zanziar na kurudi kwa majaribio na inatarajia kuanza safari zake mwezi ujao, wanaoshuhudia katika picha kutoka kulia ni Jamal Hussein Afisa Mtendaji Mkuu Citi Bank, Allan Sharra Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Precision Air na kushoto ni Rubani wa Ndege hiyo Chohan Mbarouk Mwana blog John Bukuku wa www.fullshangwe.blogspot.com akijiandaa kushuka mara baada ya ndege hiyo kurejea Dar es salaam ikitokea Zanzibar jana. Mkuu wa Mkoa wa Kagera ambaye alikuwa mgeni rasmi Mh. Mohamed Babu katikati akisubiri ndege itue ili kufanya uzinduzi rasmi kwa kukata utepe kulia ni Allan Sharra Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Precision Air kushoto ni Jamal Hussein

KELV IN IN DA HOOD

Image
SIKU MOJA MOJA NA MIMI NIKIJIWEKA SIO MBAYA

MBAVU ZANGU MIE

Image
LEO Jumapili lazima tufurahi pamoja mpenzi wa blog hii ona mwenyewe kwa macho yako

Ravalomanana ahukumiwa kifungo

Image
Rais wa Madagascar anayeishi uhamishoni, amepewa hukumu ya kifungo cha maisha jela, na kazi ngumu kwa kutoa amri ya mauaji ya wafuasi wa upinzani. Marc Ravalomanana alihukumiwa bila ya yeye kuwepo mahakamani, kufuatia mauaji yaliyotokea mwezi Februari 2009, ya watu wasiopungua 30 na walinzi wake. Bw. ravalomanana amekuwa akiishi nchini Arika Kusini tangu mezi machi mwaka 2009. Watu waliouawa walikuwa wafuasi wa Andrey Rajoelina, ambaye hivi sasa ni rais. Bw. ravalomanana alishitakiwa kwa makosa ya mauaji na kuhusika katika mauaji, pamoja na washitakiwa wengine 18, wengine pia wakiwa wanaishi uhamishoni. Wakili mtetezi wa rais wa zamani, waliondoka mahakamani muda mfupi baada ya kesi kuanza kusikilizwa, wakisema mahakama hiyo inatumiwa na utawala wa Bw. Rajoelina "Lengo ni kumhukumu ili asiweze kurejea Madagascar na kushiriki katika uchaguzi siku zijazo," wak

Poulsen awatema Tegete, Yondani, wengine watano

KOCHA wa Taifa Stars, Jan Poulsen amewaacha wachezaji saba mahiri kwenye safari ya Algeria kwa sababu ambazo ameziita kuwa za kiufundi na ushindani mkubwa kwenye kikosi chake. Kikosi hicho cha wachezaji 20 kitakachoondoka Jumanne kwenda Algeria kwa mchezo huo wa kwanza za kusaka tiketi ya kufuzu kwa fainali za Afrika mwaka 2012. Timu hiyo itaondoka kwa ndege ya Shirikika la Ndege la Qatar Airways kuelekea Algiers. Wachezaji walioachwa ni pamoja na Uhuru Seleman, Kelvin Yondani, Juma Jabu, Abdulhalim Humoud , Jerryson Tegete, Athuman Idd 'Chuji' na kipa Juma Kaseja. Poulsen alisema wachezaji hao wameachwa kwa sababu mbalimbali za kiufundi. Alisema Chuji na Kaseja bado ni majeruhi. “Chuji amepata nafuu , lakini hajakuwa na mazoezi kwa muda mrefu, siwezi kusafiri naye kwani hawezi kucheza, hali ambayo ni sawa kwa Kaseja ambaye nimempa muda zaidi wa kupona,” alisema Poulsen. Aliongeza kuwa Abdulhalim Humud, ambaye anaichezea Simba ameachwa kwa sababu ya timu yake kuwa na viungo wan

HAPPY BIRTHDAY JOH MAKINI

Image
Leo ni birthday ya Mwamba wa kaskazini kutoka Atown city,wish all da best katika Game also katika maisha yako we celebrate together

MAKAMUZI YANAELEKEA SEATTLE 28-AUG BAADA YA KASAS CITY

Image
Haya kazi kwenu wana wa EAST AFRICA mnaoishi mitaa ya SEATTLE,mwana HAULE yupo kwenu tayari kukinukisha mbaya vilivyo…show itafanyika tarehe 28 AUGUST katika ukumbi wa AFRIQ LOUNGE...usikose baab

BBA ALL STARS KURUKA BONGO FLEVA WIKI HII..

Image
Jmosi wiki hii..Dj Stive B kutoka Clouds fm atachapa ngoma kali za ukweli hasa Bongo flevaz ndani ya mjengo wa BBA All Stars na kuwarusha washiriki wote mjengoni...huu ni utaratibu mpya wa BBA All Stars mwaka huu kuwafurahisha washiriki na kuwafanya wa-enjoy weekend kila j'mosi kwa kuwaalika ma-djs mbalimbali toka nchi mbalimbali za Afrika kupiga ngoma mjengoni pale...safari hii ni zamu ya Bongo na Dj aliyebahatika kupata zali hilo ni Stive B aka Skillz...kazi kwenu fans kufuatilia nini kitajili siku hiyo

KATIZA ANGA YAO UONE SHUGHULI

Image
Ni askari wa kikosi cha kuzuia na kutuliza fujo Tanzania, Field Force Unit, (FFU) al maaruf Fanya Fujo Uone, wakiwa katika mavazi yao rasmi tayari kwa kukabiliana na purukushani zozote ambazo zinaweza kuchomoza kutokana na kutokukubaliana katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa Wabunge na Raisi.

TAHADHARI KWA WAPENDA KULA KARANGA JIANI

Image
Mfanyabiashara ndogondogo wa karanga ambaye jina lake halikujikana akiokota karanga zilizomwagika jana nje ya Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO) jijini Dar es Salaam (? na kuzichanganya kwenye zilizomo kwenye kifuko cha biashara?). Hatua hiyo inahatarisha afya za walaji kwa kuwa upo uwezekano wa kijana huyo kuziuza tena kwa wateja wake bila wao kujua kama sio salama. Mtizamaji, tizama mwelekeo wa mikono hiyo unaookota karanga, hizo zinaelekea kutupwa au kuchanganywa'mo? Ikiwa alikuwa na nia ya kuzitupa, kwa kawaida huwa tunafyagia kwa mguu kuelekea pembeni ikiwa mikono tayari imebeba kitu, ama, kile kilichobebwa huwekwa mbali na mwelekeo wa mikono au miguu huwa upande wa ardhini (kama ni kutoka kwenye sakafu) au huwa tunaacha na kusonga mbele. Matatizo ya kiafya ya magonjwa ya mlipuko vyanzo vyake ni vya aina hii kwani sehemu kinapookotwa chakula huwa imekanyagwa na viatu vilivyopita maeneo machafu sana ikiwemo vyooni na majalalani.

JAY-Z AND BEYONCE ENJOYING IN ITALY

Image
Jay-Z and his wife Beyonce are currently enjoying a romantic vacation in Italy. The couple were spotted strolling the streets of Portoferraio last Friday.

NAFAZI ZA KAZI MBALIMBALI

MANAGER TECHNICAL SERVICES SECTION Qualification: Holder of BSc. Engineering in Electronics and Telecommunications Apply: The Director General, Tanzania Meteorological Agency Box 3056, Dar es Salaam Details: Mwananchi, August 16, 2010. Deadline: September 02, 2010 HEAD LEGAL OFFICER Qualification: Holder of Bachelors of Law (LLB) Apply: The Director General, Tanzania Meteorological Agency Box 3056, Dar es Salaam Details: Mwananchi, August 16, 2010. Deadline: September 02, 2010 ENGINEER Qualification: Holder of degree in Engineering or Advanced diploma in Engineering (Telecommunications/Electronics) Apply: The Director General, Tanzania Meteorological Agency Box 3056, Dar es Salaam Details: Mwananchi, August 16, 2010. Deadline: September 02, 2010 REGISTRY CLERK Qualification: Holder of Advanced certificate of Secondary Education with passess in English Apply: The Director General, Tanzania Meteorological Agency Box 3056, Dar es Salaam Details: Mwananchi, August 16, 2010. Deadline: Septe

UCHAGUZI MKUU 2010: Mawaziri wanyakua ushindi mezani

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimezidi kujitwalia majimbo ya ubunge kabla ya upigajikura hapo Oktoba 31 mwaka huu, baada ya idadi ya wagombea wake wakiwemo mawaziri kupita kwa ushindi wa 'mezani' wa mapingamizi dhidi ya washindani wao na kuwezesha chama hicho, kuweka kibindoni majimbo 16 hadi sasa hivi. Hadi jana, CCM iliweza kujitwalia majimbo zaidi likiwemo Mlele kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, baada ya mgombea wa CUF Abasi Rashid, kujitoa kwenye mbio hizo huku katikia Jimbo la Mtama, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, akipita kwa mlango huo wa pingamizi dhidi ya Isaya Ndaka wa TLP, baada ya kukosa idadi ya wadhamini wanaohitajika. Kasi hiyo ya CCM ilizidi kuongezeka jana baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha kupita kwa mlango huo wa pingamizi dhidi ya mshindani wake kutoka Chadema Wenje Ezekie huku Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja, naye akipeta. Hadi sasa wana CCM waliotangazwa kuteuliwa wabunge na majimbo yao kwenye mabano ni

Watanzania wanaoishi nje hawatapiga kura 2010

Serikali imesema kuwa bado haijakamilisha mkakati utakaowezesha Watanzania wanaoishi nje ya nchi kupiga kura hivyo watakosa haki hiyo katika uchaguzi mkuu utakoafanyika Oktoba 31, mwaka huu. Waziri wa Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe alisema kuwa, kwa sasa bado wanalishughulikia suala hilo lakini hawawezi kupiga kura kwa sababu mchakato huo bado. “Hawawezi kupiga kura watanzania wanaoishi nje ya nchi, kwa sababu suala lao bado linafanyiwa kazi, hivyo basi hawawezi kupata nafasi ya kushiriki kwenye uchaguzi huu,”alisema Membe jana alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa, Serikali bado inaendelea kuweka mazingira yatakayowezesha watu hao kupiga kura waweze kushiriki katika uchaguzi wa mwaka 2015. Alisema pindi mchakato huo utakapokamilika, Serikali itaweka hadharani ili wadau wote wafahamu namna utakavyotekelezwa kwa kuweka mazingira huru yenye lengo la kupanua demokrasia.

HAZINA YA UTALII KISIWANI UKEREWE

Image
KATIKA POZI MASUPER STAR WA KESHO WA PANDE HIZO ZA UKEREWE MLANGO WA KUINGIA PANGO LA BENKI. KORIDO INAYOTENGANISHA PANGO LA HIFADHI (SEHEMU YA BENKI YA WATEMI) NA UKUMBI WA MAPUMZIKO. ILI KUKUZA MAENDELEO YA SEKTA YA UTALII, KAMA MCHANGO WA SEKTA HII KWA TAIFA, JUHUDI ZAIDI ZA KUBORESHA MIUNDOMBINU KATIKA VIVUTIO VYA UTALII SHURTI VIPEWE KIPAUMBELE. MUHIMU NI KWA SERIKALI NA WAENDESHA SHUGHULI ZA UTALII NCHINI, KUANDAA UTALII KWA WANANCHI ILI WAWEZE KUONA VIVUTIO NA UTAJIRI WA NCHI YAO. OF COZ' SEHEMU YA SOMO LA HISTORIA UTALII NI NJIA NYINGINE YA KUPATA ELIMU. LIKIWA NA MVUTO WA KIPEKEE HILI NI KANISA LA KWANZA LA ROMAN CATHOLIC LILILOJENGWA ENZI ZA UKOLONI KTK KISIWA CHA UKARA WILAYANI UKEREWE. H ANDEBEZYO HILL SEHEMU ILIYO JUU YA KILELE CHA KILIMA CHA PANGO LA BENKI YA WATEMI . ENEO AMBALO LILITUMIKA KWA AJILI YA ULINZI NA USALAMA WA KISIWA, KUONA MAADUI WANAOKUJA KUVAMIA NA KADHALIKA. UKISIMAMA ENEO HILI UNAONA SEHEMU KUBWA YA KISIWA CHA UKEREWE.