TENGA ATANGAZA RASMI KUTOGOMBEA TENA URAIS TFF




Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodegar Tenga amesema hawezi kugombea tena nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho hilo unaotarajia kufanyika February 24 mwaka huu.


Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Tenga amesema wakati anaingia madarakani miaka minne iliyopita alikuwa na kazi ya kufanya, ambayo ilikuwa ni kujenga taasisi ya soka nchini, na kwamba hawezi kuendelea tena kwani uongozi ni kijiti na kwamba huu sasa wakati wa kukimbizwa na mtu mwingine.

“Nimekaa madarakani kwa miaka minane kwakweli ni miaka mingi sana,tangu mwaka 2004 ambapo wakati huu kulikuwa na ajenda maalum ya kuleta mabadiliko ya msingi katika soka”alisema Tenga.

Comments


  1. Hi, Great post. I found you through the blog hop. Now following you.Please stop by and say hi when you get a chance.
    Be sure and check out my new Blog Hop that we just started, It's Weekly Goals Link Up. It's a great way to stay on track. Have a great day. :) Here's the link in case you want to check it out.
    http://lenettacarnes.blogspot.com/2013/01/weekly-goals-linkup-3.html Thanks again
    Lenetta

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA