DONALD TRUMP ASHINDA NEVADA


Donald-Trump
Mgombea wa urais wa Chama cha Republican, Donald Trump ameshinda katika Jimbo la Nevada nchini Marekani, na kuzidi kuimarisha uongozi wake katika mchujo wa kuwania tiketi ya chama hicho.
Tajiri huyo sasa ameshinda mara tatu, kufuatia ushindi wake katika Jimbo la New Hampshire na Carolina Kusini.
Seneta Marco Rubio na Ted Cruz ambao wamekuwa wakishambuliana wiki hii wanapigania nafasi ya pili.
Maofisa wa chama hicho wamesema wamekuwa wakichunguza ripoti za watu kupiga kura mara mbili huku eneo moja likidaiwa kuwa na vifaa vichache vya kupigia kura.
Baadhi ya watu waliojitolea pia walidaiwa kuvaa nguo zenye picha za bwana Trump, lakini maofisa wamesema kuwa hatua hiyo siyo kinyume na sheria.BBC

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA