TTCL yakanusha taarifa za mfumo wake wa mawasiliano kuingiliwa na kudukuliwa

Meneja wa Kitengo cha Usalama Mifumo ya Mawasiliano ya TTCL, Lina Rujweka akifafanua jambo kwenye mkutano na vyombo vya habari leo.
KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) imekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa mfumo wa mawasiliano wa kampuni hiyo umeingiliwa na wadukuzi. Taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam na Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Nicodemus Thomas Mushi alisema taarifa zinazotolewa si za kweli hivyo kuwataka wateja wao wazipuuze.

“...Tunapenda kuwathibithia Wateja wetu wote wa ndani na nje ya nchi, wadau wetu na Umma kwa ujumla kwamba, taarifa hizi si sahihi, na kwamba mifumo yetu ya Mawasiliano ya TTCL ipo salama, huduma zetu zote zipo thabiti na mpaka sasa tunapotoa taarifa hii, hakuna uhalifu wowote uliofanyika kwa sisi wenyewe kama Kampuni wala kwa mteja wetu yeyote,” alisema Thomas Mushi.

Aidha, tunapenda kuwathibitishia kuwa, taarifa za Wateja wetu wote ikiwemo Serikali , Idara, Wakala na Taasisi za Umma, Taasisi za fedha, Mashirika, Makampuni na Watu binafsi zipo salama kabisa. Ukweli huu unathibitishwa na Wateja wao pia kwani hadi sasa, hakuna hata mmoja aliyeleta taarifa za kukosa huduma ama kupata athari zozote kutokana na tetesi hizo.

Hata hivyo, alisema pamoja na taarifa hizo, Wataalamu wa kampuni hiyo wanaendelea kuwa macho kwa muda wote, ili kuhakikisha kuwa, wanafanyia kazi kila taarifa ama tishio la kiusalama linaloweza kujitokeza katika mfumo wao.

“TTCL inaendelea kuwaomba Umma na Wateja wetu wote kuendelea na majukumu yao kama kawaida bila wasiwasi wowote. TCCL inawaleta Karibu.” Alisema Thomas Mushi.

Kwa upande wake Meneja wa Kitengo cha Usalama Mifumo ya Mawasiliano ya TTCL, Lina Rujweka alisema kitengo chao baada ya tetesi hizo kimefanya uchunguzi wa kina na hakuna ashirio lolote la mifumo yao kuingiliwa (kudukuliwa) kama ilivyoelezwa.

Alisema kitengo hicho kina wataalam ambao muda wote wapo kazini kufuatilia ufanisi wa mfumo wa mawasiliano wa kampuni yao hivyo kuwaondoa hofu wateja wao.

“... Baada ya taarifa hizo Kitengo cha Usalama wa Mifumo ya Mawasiliano ya Kampuni ya TTCL kiliingia kazini ili kubaini ukweli wa taarifa hizo na kufanya majaribio ya kitaalamu ili kuthibitisha usalama wa mifumo yetu. Baada ya utafiti wa kina na majaribio ya kitaalamu, tunapenda kuwathibithia Wateja wetu wote wa ndani na nje ya nchi, wadau wetu na Umma kwa ujumla kwamba, taarifa hizi si sahihi...” alisema.

Meneja Uhusiano wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas Mushi akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam kukanusha taarifa za kampuni hiyo kudukuliwa.
Baadhi ya wanahabari katika mkutano leo na kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Anonymous Leaks Details for 64,000 Tanzania Telecommunications Company Employees

OpAfrica continues to make new victims, it's Tanzania's turn

Feb 15, 2016 22:31 GMT  ·  By  
Barely a day has passed since the most recent Anonymous attack and the hacktivists are back with another one, this time against Tanzania Telecommunications Company Limited (TTCL), a state-owned company that provides fixed basic telephone services in Tanzania and Zanzibar.
As with the most recent Anonymous-attributed attacks, the responsibility for this attack is on the World Hacker Team, one of the group's most active subdivisions.
The hackers dumped details for over 64,000 TTCL employees, data which includes real names, email addresses, telephone numbers, the department in which employees work, and their respective job title.
The data seems to be stolen from the company's website, because outside employee details, the hackers also dumped data for users that had an account on the site, information that included usernames and password hashes.
If you're wondering why the hackers did it, the answer is #OpAfrica, a campaign that the Anonymous hacker collective launched at the start of February to bring the world's attention to the situation of child labor and government corruption to African countries.
Many have argued that the group isn't actually helping since it's not doing anything except to hack government agencies and state-owned companies that have weak security measures, and then dump data of innocent people online, exposing them to various types of dangers.
Right now, you can see public opinion swinging against #OpAfrica as the hacks seem to cause more problems for regular users rather to the compromised governments.
UPDATE 1: TTCL has denied that hackers breached its servers. The company said it only has around 1,600 employees, not 64,000. We looked at the data and discovered numerous duplicate entries, which validates their claim, and we'll be more than happy to point TTCL's team to the links if they would have answered our initial email.
UPDATE 2: Some more clarifications on our initial report. Before publishing, we've spent quite some time searching through the data and identifying if the details led back to real TTCL employees, but we didn't check for duplicate entries, since we haven't seen any duplicates from the World Hacker Team group until now. The real headcount is 2,287. We've also sent a second email to TTCL, this time containing links to the data dump so they could investigate and discover what the group accessed.
 Links to the data dumps (edited)
Links to the data dumps (edited)
Source: news.softpedia.com

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA