WAZIRI NDALICHAKO ASITISHA MKATABA WA MKURUGENZI BODI YA MIKOPO NA KUSIMAMISHA WAKURUGENZI 3 HESLB

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amevunja mkataba wa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) nchini, George Nyategi na kuwasimamisha kazi wakurugenzi wengine watatu huku akitaka uchunguzi ufanyike haraka.

Mkataba wa Bw. Nyageti uliopaswa kuisha tarehe 31/08/2016 umevunjwa leo na kuamriwa alipwe mshahara wa mwezi mmoja kwa mujibu wa kifungu namba 50,03,a cha kanuni za kudumu.

Wengine waliokumbwa na fagio hilo ni pamoja na Mkurugenzi wa Fedha, Bw. Yusuph Kisare, Juma Chagonja, Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo na Bw. Onesmo Laizer na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo, Yusuf Kisare.

Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na kuwepo kwa ukiukwaji wa utoaji wa mikopo pamoja na ucheleweshaji usio na sababu za msingi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Profesa Ndalichako amesema kuwa bodi ya mikopo imekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wanafunzi wanaostahili kupata mikopo na kufanya kwao kuweza kupata mikopo mpaka waandamane wizarani kwa kusababishwa na watu wachache wa bodi hiyo.

Profesa Ndalichako, amesema katika udhaifu wa utendaji huo ni pamoja na ulipaji wa mikopo kwa wanafunzi 23 waliolipwa katika vyuo viwili tofauti kwa miaka mitatu mfululizo kwa chuo cha kwanza zililipwa zaidi ya sh.milioni 653 na chuo cha pili ni zaidi ya sh. milioni 147.

Amesema baadhi ya wanafunzi ambao walikwenda kusoma nchini Algeria wamekuwa wakiendelea kulipwa fedha wakati mkataba wao umekwisha kwa kipindi cha miaka saba.

Profesa Ndalichako amesema wanafunzi 169 walipata mikopo katika vyuo viwili tofauti kwa miaka mitatu mfululizo na kulipa chuo cha kwanza zaidi ya sh.milioni 658 na chuo cha pili zaidi ya sh. milioni 665 na wanafunzi 55 walioacha masomo walilipwa zaidi ya sh.milioni 136 huku wanafunzi 343 wasiokuwa na usajili kwenye vyuo husika walilipwa zaidi ya sh.milioni 342.

Aliongeza kuwa zaidi ya sh.milioni 159 zililipwa kwa wanafunzi 306 zaidi ya kiwango kilichobainishwa kutokana na muongozo wa upangaji na ukopeshaji wa mwaka 2008/2009 na 2009/2010.

Aidha amesema kuwa wanafunzi 77 walipatiwa mikopo kwenye vyuo vya ndani na nje ya nchi kwa wakati mmoja ambapo walilipwa zaidi ya sh.milioni 467 kwa vyuo nje na zaidi ya sh.milioni 123 kwa vyuo ndani pamoja na wanafunzi 19,348 walipata mikopo bila kupitiwa na kamati ya mikopo jambo ambalo ni kinyume na kanuni na 8ya kanuni za mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Hatahivyo amesema wanafunzi 54,299 walipangiwa mikopo wakati hawakuwa wameomba ambapo walilipwa zaidi y ash.milioni 207 ambazo zilipelekwa kwenye vyuo sita.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA