TAARIFA RASMI KUTOKA KWA RAIS WA SERIKALI YA WANAFUNZI SAUTSO

KUTOKA KWA RAIS WA SAUTSO MH.MALISA GODLISTEN 
Kwa takribani wiki mbili sasa imekuwepo hali ya sintofahamu kuhusiana na fedha za Field na baadhi ya watu wameanza kupika taarifa za uongo na uzushi ili kupotosha kwa makusudi.

Ukweli ni kuwa sisi kama serikali tumejitahidi kwa kadri ya uwezo wetu kuhakikisha fedha hizo zinapatikana kwa wakati. Tar 3 hadi 5 mwezi huu nilikuwa Bodi kufuatilia fedha hizo. Ikumbukwe ilikuwa ni siku moja tu baada ya kumaliza mitihani. Nilifanya hivyo ili kuepusha usumbufu ambao ungeweza kujitokeza baadae.

Lakini Bodi hawakuwa na hela hivyo wakahidi kutupatia fedha hizo mara tu watakapopokea kutoka Hazina. Tukaendelea kuwasiliana na Bodi ambao waliendelea kudai hawana fedha. Kufikia tar.19/07/2012 nikiongozana na waziri wa mikopo tukalazimika kwenda Bodi kwa dharura.

Lakini hata baada ya kufika bodi jibu lilikuwa ni lilelile kuwa hawana fedha. Lakini mbaya zaidi hatukuwemo kwenye list ya vyuo vilivyopaswa kulipwa mwezi huu. So kwa msaada wa Mh.Ezekia Wenje tukawasiliana na Mkurugenzi wa Bodi Mr.Nyatega ili tuwe kwenye payroll ya mwezi huu.

Lakini pamoja na kuwepo kwenye list but changamoto ikabaki palepale kuwa Bodi hawana fedha. So tukalazimika kwenda Hazina ili kuomba serikali kupeleka fedha Bodi. Baadae tukawasiliana na Naibu Waziri wa Elimu Mh.Mulugo ili ajaribu kupush Hazina wapeleke fedha Bodi.

Baada ya support kubwa kutoka kwa Mh.Wenje tukapata taarifa kuwa Hazina wamepeleka fedha Bodi tar.21, so tar.23 tukaenda tena Bodi ili kuziwahi kabla hazijapelekwa vyuo vingine.

Waziri wa mikopo akapambana, tar.24 tukaandikiwa Vocher, tar.26 Bodi wakahakiki malipo. Tar.27 Bodi wakatuma payroll kwa EMS. Tar.28 tukaanza kusort majina ili kuweza kuwalipa. Kwa kuwa kazi hiyo ni kubwa Loan Officer akalazimika kuifanya hadi jumapili. Then leo tukafanikiwa kuwalipa BAED, BAEC, ADA, ADPLM na Bphl.

Kesho tunategemea kuwalipa BAMC, LLB 2, and if possible PR. Then course nyingine zitamaliziwa jumatano. Kimsingi tumefanya juhudi kubwa sana kuhakikisha mnapata fedha zenu. Bila juhudi binafsi ambazo zilimhusisha kwa karibu Waziri wa mikopo Bw.Byera na Mh.Wenje, kulikuwa na possibility ya fedha hizi kuchelewa zaidi.

Lakini unfortunately wakati tuko busy kupigania haki yenu, wapo wengine waliokuwa busy kuandaa Propaganda na kupotosha kwa makusudi. Wakati mwingine tumelazimika kutokula au kulala ili kupigania haki yenu. Kwa mfano, LLB2 ambao hawajaahi kupewa hela ya field, mwaka huu tulipeleka special request na fedha zao zimekuja, so tutawalipa kesho. Hizi ni juhudi ambazo zinapaswa kupongezwa na si kueneza propaganda za kupotosha na kulalamika tu....!!!

Nashauri watu watafute habari za uhakika kuliko kupotosha kwa makusudi kwa manufaa ya kisiasa. Pongezi kwa Loan Officer Mr.Musa kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mnalipwa kwa wakati, Waziri wa Mikopo Mr.Byera na Mbunge wa Nyamagana Mh.Wenje kwa msaada wake wa hali na mali na makamanda wengine waliofanikisha suala hili. Nawatakia likizo njema.

Comments

  1. Naona umeongelea LLB2 habari gani juu y LLB3?

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA