WALIMU WASHINIKIZA KUGOMA MKOANI MARA HAPO KESHO


Shomari Binda,
Musoma

Chama cha walimu (CWT) Mkoa wa Mara kimewasihii walimu kutohadaika na kauli ya Serikali ya lkuwataka kutokugoma kwani haki zao bila kuchua hatua hutua hiyo hazitatimizwa kwa wakati.

CWT imesema upatikanaji wa maslahi bora ya kazi yatapatikana kwa kushirikiana katika mgomo utakaoanza kesho ili Serikali ione umuhimu wa madai yao ambayo wamekuwa wakiyadai kwa muda mrefu sasa bila kupatiwa ufumbuzi.

Katibu wa CWT Mkoa wa Mara Fatuma Bakari amesema walimu wasiwe waoga kutetea haki zao kwani mgomo huo huko kisheria na kinachofanywa na Serikali ni vitisho kwao ambavyo amesema havina msingi.

Bakari amewakumbusha walimu kuwa madai yao ya maslahi bora ni ya muda mrefu huku akihituhumu Serikali kuendelea kuyapuuzia na kuwafanya kuishi maisha duni na kifukara licha ya kufanya kazi kubwa nayakujituma.

Uchunguzi uliofanywa na BINDA NEWS Mjini Musoma umeonyesha kuwa mgomo huo hupo kesho na walimu wengi wamenukuliwa wakisema wako tayari kugoma ili kuishinikiza Serikali kutatua kero zao wanazozidai.

Walimu hao wamesema kamwe hawawezi kuwasaliti viongozi wao wa Kitaifa waliowachagua na kuwaachia vita hiyo ya madai ya msingi wapigane wenyewe kama vile wanapigania maslahi yao binafsi.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA