Rais Kikwete aanza ziara ya nchi tatu Ulaya.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Kikwete aanza ziara ya nchi tatu Ulaya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatatu, Juni Mosi, 2015 ameanza ziara rasmi ya wiki moja katika nchi tatu za Ulaya kwa mwaliko wa viongozi wa nchi hizo.

Rais Kikwete ambaye aliondoka nchini usiku wa jana, Jumapili, Mei 31, 2013 baada ya kumaliza kuendesha Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Burundi ameanzia ziara yake katika Finland ambako atakaa kwa siku tatu.
  
Baadaye, Rais Kikwete atatembelea nchi za Sweden na Uholanzi kabla ya kurejea nyumbani.

Katika Finland, Rais Kikwete miongoni mwa mambo mengine kesho Jumanne, Juni 2, 2015, atafanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali na Rais wa nchi hiyo na baadaye atatembelea Bunge la nchi hiyo ambako atafanya mazungumzo na Wabunge.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

1 Juni, 2015

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA