AY AAMPLIFY KUHUSU KOLABO ZA TYGA WA YOUNG MONEY & YOUNG JOC!



Tyga & Ay
Siku nne baada ya kuthibitisha kupiga kolabo na wakali kutoka Jamaica Tanto Metro na Devonte, Ambewe Yessaya AY amethibitisha kwamba kolabo aliyoipiga mwanzo na Young Joc wa Bad Boy imemalizika, na kilichobaki ni Video tu.
Amesema ” Audio yote iko sawa, yeye ndio alianza kuirekodi kabla yangu mimi, vilevile Audio nyingine ambayo inarekodiwa sasa hivi ni ya TYGA ya Young Money ndio kolabo ambayo nina hamu nayo sana, ilikua irekodiwe mwezi huu wa february lakini imesogezwa mbele na sasa itafanyika kabla ya june mwaka huu, nikitulia naweza kuianza may na kila kitu kiko kwenye mstari”


story na picha  ni kwa hisani ya http://millardayo.com

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA