WALIMU WAPYA WAANDAMANA RORYA

ZAIDI ya walimu wapya  40 wameandana na kulala katika ofisi za Halmashauri ya Wilaya Rorya zilizoko Ingiri juu kushinikiza kulipwa pesa yote ya kujikimu ya siku saba.

Hali hiyo imekuja baada ya walimu hao kubaini kuwa katika Wilaya zingine wenzao walilipwa kiasi tofauti na wao.

Wakizungumza na waandishi wa habari mapema asubuhi jana walimu hao walieleza kuwa kulipwa pesa ya siku nne kunawafanya washindwe kuandaa maisha yao mapya vizuri na pesa hiyo haitatoshi kulingana na mazingira yalivyo Wilayani humo.

“Tuliamua kutembea kwa miguu na kuja kulala hapa ili uongozi uone kuwa hatukubaliani ha kiasi hicho cha pesa ya kujikimu wanachokitoa kwetu” alisema mmjoja wa walimu hao ambaye hakutaka jina lake kutajwa gazetini.

Walisema kuwa kati ya walimu 160 walioajiriwa katika Halimashauri hiyo wakiwemo walimu wachache wa shule za sekondari, baadhi yao walipokea kiasi cha shilingi 140,000 ambacho ni cha siku nne na waliobaki walikataa wakidai walipwe pesa yote ya siku saba.

“Mimi nina mke na sina chombo cha ndani hata kimoja wakinipa shilingi 140,000/- kitanisaidia nini na  bei ya vitu iko juu nitaishije sina kitu ndani? Alihoji Mwalimu Musa Abdi.

Kutokana na maandamano hayo uongozi wote wa Wilaya hiyo ulifanya kikao na walimu hao na kuwaomba wapokee kiasi hicho ambachokipo na watalipwa kwa kuwa hakuna pesa ya kutosha katika halmashauri hiyo.

Afisa elimu wa Wilaya hiyo Michael Igogo alisema kuwa wanafanya mazungumzo na RAS na TAMISEMI kuona namna ya kutatua tatizo hilo linalowakabili, na kuongeza kuwa hoja yao ni ya msingi.

“Hoja zao ni kuwa kwa nini hawalipwi pesa zote kama Wilaya zingine, lakini Wilaya hizo zina mapato makubwa.Hata hivyo tumeamua kuwalipa sawa wote shilingi 245,000/-“ alisema Igogo.

Ofisa huyo aliongeza kuwa kati ya walimu waliopangiwa Wilayani humo wengine walipelekewa pesa zao vituoni mwao ili kuondoa usumbufu wa wao kufuatilia pesa hizo ofisini badala ya kuwahudumia wanafunzi.

“Hawa ni wale waliochelewa kuripoti na kutokana na kuwa hatuna pesa za kutosha tumeamua kuwapa kiasi hicho cha siku nne halfu tutawamalizia kiasi cha siku tatu baada ya kurekebisha mambo” alisema afisa Elimu huyo.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA