Kanda ya ngono yamtia mashakani mwalimu mkuu


Shule iliyokumbwa na kashfa

Mwalimu mkuu wa shule moja ya upili nchini Uingereza ameachishwa kazi kufuatia utata kuhusu kanda ya ngono inayodaiwa kurekodiwa shuleni humo.
Mwenyekiti wa bodi ya shule alimwachisha kazi mwa muda mwalimu mkuu Graham Daniels na mfanyakazi mwingine wa shule ambaye jina lake halikutajwa baada ya malalamiko kutolewa kuwahusu wawili hao.

Kuachishwa kazi kwa mwalimu huyo kulitokea baada ya wanafunzi kusambaza kanda hiyo kwa mitandao ya kijamii. Kanda hiyo ilikuwa na sauti za watu wawili wakijihusisha na ngono katika chumba kimoja cha shule hiyo.
Hata hivyo wakuu wa bodi walisema kuwa shughuli za masomo zinaendelea kama kawaida.
Mkuu wa bodi alisema: "shule imepokea malalamiko ambayo hayakumtaja mtu yeyote lakini kufuatia madai hayo uchunguzi utafanywa.''

Mwalimu mkuu na mfanyakazi mwingine wa shule wameachishwa kazi kutokana na madai hayo.

source:bbc swahili.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA