DC MAKONDA AKUTANA NA VIJANA WASIO NA AJIRA NA KUWAUNGANISHA, KUBUNI MIRADI YA KIUCHUMI ILI KUPUNGUZA TATIZO LA AJIRA

????????????????????????????????????

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akizungumza na vijana  ambao hawana ajira  wenye elimu tofauti  katika viwanja vya Leaders  jijini Dar es salaam, ambapo amekutana na vijana hao  ili kuzungumza nao kwa ajili ya kutatua tatizo lao lao la ajira .

DC Makonda amesema lengo la kuwaita vijana hao ilikuwa ni kuwakutanisha  wafahamiane na wabadilishane mawasiliano lakini pia wataunda vikundi vyao kulingana na taaluma zao na kila kundi litaandika miradi ipatayo mitano ili tuweze kuifanyia kazi kwa kuwatafutia mitaji au ufadhili baada ya miradi yao kubuniwa 
Ameongeza kwamba mpango huu utapunguza vijana kukaa bila kazi na kuingia katika vishawishi vya mimba kwa wasichana na na matukio yasiyo mema katika jamii. kama vile uhalifu na mengine mengi.

Lakini pia amesema kuna makampuni mengi yameahidi kuchukua vijana wenye uwezo wa kufanya kazi kwani kwa kuwaunganisha vijana hao litakuwa ni jambo rahisi kupata wafanyakazi wa kuajiri , ikiwa ni pamoja na kuchukua vijana watakaofanya kazi kwa kujitolea na baada ya kuonyesha uwezo kazini wao wataajiriwa na mashirika au taasisi husika.

????????????????????????????????????
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akizungumza na vijana hao kwenye viwanja vya Leaders
????????????????????????????????????
Baadhi ya vijana wakiwa katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akizungumza na baadhi ya waandishi wa habari kutoka kituo cha televisheni cha Chanel Ten.

chanzo:fullshangweblog.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA