Al Shabaab wadai kuteka askari wa Uganda


Wapiganaji wa Al Shabaab
Wapiganaji wa kiislamu wa Alshabab wamesema katika maneno yao kuwa linawashikilia mateka wa kivita kutoka Uganda waliowateka wakati wa mashambulizi ya wiki iliyopita.
Uganda imesema kuwa wanajeshi kumi na mbili waliokuwa chini ya jeshi la umoja wa Afrika wakilinda amani nchini Somalia waliuawa katika shambulio hilo kwenye ngome yao iliyopo kusini mwa nchi hiyo.
Wanadiplomasia wa nchi za magharibi wamesema kuwa zaidi ya wanajeshi mia moja wa Uganda aidha wamekufa au hawajulikani walipo.
Afisa mmoja wa kundi la Alshabab amesema wanajeshi hao wa Uganda wapo salama na wana afya njema.
Hakuweza kusema ni wangapi walioshilikiliwa ama nini kinaweza kutokea kwa mateka hao.
Amesema Uganda imefanya makosa ilipotamka juma lililopita kuwa wanajeshi wake wote wamehesabiwa.
Katika siku kadhaa zilizopita wanamgambo hao wa Al Shabaab walitumia picha za askari waliofariki wa Umoja wa Afrika na vifaa vyao katika kuendeleza propaganda zao.
Ingawa kundi hilo hivi karibuni limepoteza maeneo mengi nchini Somalia, juma lililopita lilikamata miji miwili iliyokuwa iliyoachwa na jeshi la umoja wa Afrika.BBC

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA