MAGUFULI ATIKISA MIKOA YA GEITA NA SHINYANGA

magufuli akifanya mkutano wake wa mwisho mjini kahama leo katika viwanja vya UWT CCM Kahama
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk Jonh Pombe Magufuli akifanya mkutano wa kampeni katika viwanja vya UWT CCM, Kahama.
Mjumbe wa kamati kuu ya ccm na mwenyekiti wa jumuiya ya wazaz ccm, Abdalah Bulembo akiwataka wananchi kuichagua ccm Ktika uchaguz mkuu ujao
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM, Abdalah Bulembo akiwataka wananchi kumchagua Magufuli.
Samuel sitta akiwaomba wananch waliokusanyika viwanja vya UWT CCM Kahama kumchagua magufuli
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Msitaafu, Samuel Sitta akimnadi Magufuli.
katibu mwenez wa chadema Musa Dida akirudisha kadi nya chadema ccm na kuvua gwanda
Katibu Mwenezi wa Chadema, Musa Dida akirudisha kadi ya chama chake, kuvua gwanda na kuchukua kadi ya CCM.(P.T)
sehemu ya wakazi waliofurika katika viwanja vya UWT Kahama wakiwa na mabango
Sehemu ya wakazi waliofurika katika viwanja vya UWT Kahama wakiwa na mabango ya kumfagilia Magufuli.
wakaz wa Bulungwa wakimsikiza magufuli baada ya kumsimamisha barabarani (1)
Wakazi wa kijiji cha Bulungwa wakimsikiza Magufuli baada ya kumsimamisha barabarani
wakaz wa igulwa (1)
wakaz wa igulwa (2)
Wakazi wa kijiji cha Igulwa
wakazi wa mbogwe wakimsikiliza magufuli
Wakazi wa Mbogwe wakimsikiliza Magufuli
Wakazi wa mgodi wa nyarugusu (1) 
Wakazi wa mgodi wa nyarugusu (2)
Wakazi wa mgodi wa Nyarugusu
yamoto wakifanya yao viwanja vya UWT Kahama
Kundi la waimbaji wa Yamoto Bendi wakifanya yao viwanja vya UWT Kahama.
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Pombe Magufuli leo ameitikisa mikoa ya Mikoa ya Geita na Shinyanga kwa kufanya mikutano 14 ya kampeni katika maeneo tofauti .
Dk Magufuli alifanya mikutano katika vijiji saba vya mkoa wa Geita na mikutano mingine saba aliifanya mkoani Shinyanga ukiwemo mkutano uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi kwenye viwanja vya UWT CCM vilivyopo Kahama Mjini.
Katika kampeni hizo wanachama zaidi ya 20 kutoka vyama pinzani vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi Mkuu walisalimisha kadi zao kwa Magufuli na kujiunga CCM. Wanachama hao waliahidi kumuunga mkono Magufuli kwa kumpa kura zao urais pamoja na wabunge na madiwani wa CCM.
Katika kampeni zake ambapo leo Magufuli kakribani maeneo yote aliyofanya mikutano yanawahusu wachimbaji wa madini. Magufuli aliwaahidi neema wachimbaji hao kuwa, endapo watamchagua na kufanikisha kuwa rais wa Tanzania, atawamilikisha machimbo mapya watakayovumbua.
Kuhusu wafugaji katika maeneo hayo, Magufuli aliwaahidi kuwatafutia wawekezaji wa viwanda vya ngozi ili kupandisha thamani ya mifugo yao. Aidha Magufuli aliwaambia wakulima wa pamba kuwa, endapo watamchagua yeye, madiwani na wabunge wa CCM, ataanzisha viwanda vya nyuzi na vitambaa hivyo akawataka wananchi hao wakae mkao wa kimaendeleo.
Mgombea huyo leo kampeni zake ziliishia uwanja wa UWT CCM Kahama Mjini ambapo kesho zinatarajia kuishia Shinyanga Mjini.
(PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS/GPL ALIYEKO SHINYANGA)

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA