Uchina yafaa kueleza sera zake za uchumi


Wizara ya fedha ya Marekani imesema inaonesha Uchina imefahamu kwamba inahitaji kuimarisha mawasiliano kuhusu sera zake za uchumi baada ya mtafaruku wa mwezi uliopita katika masoko ya fedha ya kimataifa.
Taarifa hiyo inafuatia mazungumzo baina ya waziri wa fedha wa Marekani, Jack Lew, na mwenzake wa Uchina, Lou Jiwei, kando ya mkutano wa mataifa 20 yenye uchumi mkubwa kabisa duniani - G20.
Bwana Lew piya aliisihi Uchina isipunguze thamani ya sarafu yake, ili kufanya bidhaa inazosafirisha nje kuwa rahisi.
Mazungumzo hayo yanayofanywa Ankara, Uturuki, yaliangalia haja ya kukuza uchumi na kuzidisha imani katika masoko baada ya bei za hisa kuporomoka mwezi uliopita, huko Uchina na sehemu nyingi za dunia.BBC

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA