URENO KUTOKA ‘BEST LOSER’ HADI MABINGWA WA EURO 2016


Portugal-champions
Ureno wameweza kuikabili Ufaransa na kuichapa bao 1-0 kwenye mchezo wa fainali ya michuano ya Euro 2016 na kushinda taji lao kubwa kwa mara ya kwanza bila ya nahodha wao Cristiano Ronaldo aliyetoka mapema kipindi cha kwanza baada ya kuumia. Loser

Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid alibebwa kwenye stretcher huku akibubujikwa na machozi dakika ya 25 ya mchezo dakika nane baada ya kuumia goti alipopambana na mfaransa Dimitri Payet.

Ufaransa timu ambayo ilipewa nafasi kubwa ya kushinda ubingwa huo, walishindwa kupata bao kwa kutumia faida ya kukosekana kwa Ronaldo uwanjani licha ya kukaribi kupata bao dakika za lala salama kupitia kwa Andre-Pierre Gignac aliyeingia kutoka benchi ambapo shuti lake liligonga mwamba.

Raphael Guerreiro alipiga mpira wa adhabu ndogo uliogonga mtambaa panya lakini sekunde chache baada ye Eder aliachia shuti la chinichini akiwa umbali wa mita 25 kutoka golini lililomshinda golikipa wa Ufaransa Hugo Lloris na kuzama wavuni.

Ronaldo ambaye alikuwa akiwahamasisha wachezaji wenzake wakati wa mapumziko kabla ya dakika 30 za nyongeza, alikuwa akitekeleza majukumu ya benchi la ufundi sambamba na kocha Fernando Santos hasa wakati wa dakika za mwisho na alishindwa kuzuia machozi ya furaha baada ya filimbi ya mwisho kabla ya kunyanyua ndoo aliyoisubiri kwa muda mrefu akiwa na timu yake ya taifa ya Ureno.

Matukio katika namba
35: Ureno wameshinda taji lao la kwanza la Ulaya baada ya mechi 35 kwenye mashindano hayo.
10: Ureno ni taifa la kumi tofauti kushinda kombe la mataifa ya Ulaya.

6: Eder ni mchezaji wa sita kufunga goli kwenye michuano ya Ulaya akitoea benchi anaungana na Oliver Bierhoff, Sylvain Wiltord, David Trezeguet, Juan Mata pamoja na Fernando Torres.
3: Ureno imekuwa nchi ya kwanza kwenye michuano ya Ulaya kucheza mechi tatu hadi dakika 30 za nyongeza ndani ya msimu mmoja wa mashindano.

80: timu ya taifa ya Ureno ilifanikiwa kupiga shuti lake on target dakika ya 80, muda mrefu zaidi kwenye fainali za michuano ya Ulaya. Chanzo..shaffihdauda.com

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA