DR SLAA: vichwa vyetu vina TATIZO

 

Dr Wilbroad Slaa
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) DR Wilbrod Slaa, ameitaka serikali kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu hali mbaya ya kifedha ambayo inalikabili taifa hivi sasa kwa kupungua kwa mapato ya ndani na ya nje, ikilinganishwa na bajeti iliyopitishwa kufafanua mkakati wa kuongeza uzalishaji na kupunguza matumizi ya serikali.
 
Kwenye sentensi nyingine, Dr slaa ameitaka CCM, serikali na vyombo vya dola kubadilika 2012 ili kuepusha nchi kuingia katika malumbano na migogoro ya kijamii, ambapo ishu nyingine aliyoizungumzia baada ya kukutana na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, ni kuitaka serikali kushughulikia chanzo cha matatizo ya wananchi, na sio kushughulikia matawi ya matatizo hayo.
 
Hakusahau kuzungumzia ishu ya wakazi wanaoishi mabondeni dar es salaam, ambao zaidi ya siku 10 zilizopita, walikumbwa na mafuriko yaliyopoteza maisha ya zaidi ya watu 40, ambapo amesema “ni aibu juzi TABATA ndege ya polisi inapita badala ya kuokoa watu, inakagua tu na kuondoka, VICHWA VYETU VINA TATIZO, rais anasema wenye nyumba watafidiwa, je na wale wapangaji? wamepoteza mali na watoto….. hii ndio aina ya serikali tuliyonayo, kama tunaweza kuweka mabomu makubwa ya kuwapiga kina Dr Slaa tunashindwa kununua vifaa kama helkopta na boti za kuokoa rais? serikali inatakiwa kushughulikia chanzo cha matatizo” – DR SLAA

Comments

  1. this is t bro iwould like to share ideas throu my blog gmarandu.blogspot.com

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA