Bomoabomoa yaendelea: Nyumba zaidi ya 400 Kibamba zavunjwa

Wakazi waliojenga eneo la Iloganzila Jimbo la Kibamba Dar es salaam leo wamebomolewa nyumba zao ambazo ni zaidi ya nyumba 400, zoezi hilo limekuja baada ya amri iliyotolewa na Mahakama Kuu juzi.
WANANCHI kadhaa waliojenga eneo la Iloganzila Jimbo la Kibamba leo wamefikwa na majonzi baada ya nyumba zaidi 400 kukumbwa na mbomoamboa.
Taarifa zinasema, zoezi la bomoabomoa hiyo lilikuwa ni utekelezaji wa amri iliyotolewa na Mahakama Kuu, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Eneo hilo lenye ukubwa wa heka 33, linadaiwa kuwa ni mali ya Henry Kashangaki na limekuwa katika mgogoro tangu 1997 baada ya kundi la watu wapato 11 kuvamia na kuanza kujenga nyumba na kuwauzia wananchi wengine.

Inaarifiwa kwamba baada ya eneo hilo kuvamiwa mmiliki wake aliamua kwenda mahakamani na kuwashtaki Shaha Matibwa na wenzake kumi.

Kesi hiyo iliendeshwa kwa muda wa miaka mitano na mwaka 2010 hukumu ilitolewa, Kashangaki na Matibwa walionekana wana haki ya kumiliki hivyo walitakiwa kugawana.

Hata hivyo Kashangaki hakuridhika na hukumu hiyo na kukata rufaa na kwenda Mahakama Kuu, January 2016 kesi hiyo ilitolewa hukumu na Kashangaki alishinda.

Taarifa zinasema kuwa Mahakama kuu ndiyo ilitoa amri nyumba zivunjwe ili kumpisha Kashangaki.


Taarifa zinasema eneo hilo lenye ukubwa wa heka 33, mali ya Henry Kashangaki lilikuwa na mgogoro tangu 1997 baada ya kundi la watu 11 kuvamia na kuanza kujenga nyumba na kuwauzia wananchi wengine.


Baada ya eneo hilo kuvamiwa mmiliki wake aliamua kwenda mahakamani na kuwashtaki Shaha Matibwa na wenzake kumi, kesi hiyo iliendeshwa kwa muda wa miaka mitano na mwaka 2010 hukumu ilitolewa na Kashangaki na Matibwa walionekana wana haki ya kumiliki hivyo walitakiwa kugawana.


Hata hivyo, Kashangaki hakuridhika na hukumu hiyo na kukata rufaa na kwenda Mahakama Kuu, January 2016 kesi hiyo ilitolewa hukumu na Kashangaki alishinda, hivyo juzi Mahakama hiyo ilitoa amri nyumba zivunjwe ili kumpisha mwenye eneo lake.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA