WAHITIMU CHUO KIKUU CHA KANISA KATOLIKI CHA SAYANSI ZA AFYA BUGANDO WAPOKEA NONDO ZAO


"Anayetimiza wajibu wake hupata furaha ya moyoni" Kauli ya Mgeni rasmi Mhasham Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha SAUTI Agustin Shayo.

Meza kuu.

Licha ya juhudi za nchi kupata wataalamu wake kwenye sekta ya afya imeanza zamani lakini mpaka sasa idadi ya wataalamu kwenye sekta hiyo hairidhishi hivyo jitihada za dhati zinahitajika kukidhi mahitaji ya hospitali zetu.

Takwimu zinaonyesha kwamba karibu 60% ya wafanyakazi wanaohitajika kwenye sekta hii hawapo hivyo maamuzi ya kuanzishwa kwa chuo hiki cha kufundisha madaktari yalilenga kuchangia kupunguza pengo hilo. Big up kwa BUGANDO.

Rais wa Touch Foundation Mr Bryan Lowell akisema machache kwenye mahafali hayo. Ni mfuko ulio wawezesha wahitimu wengi kulipia ada za masomo.

Since the establishment of this medical school a total of 556 students have graduated, 337 in Diploma Programmes, 144 in the MD Course, 33 in Masters programmes and one in PhD programme.

Sehemu waliyo keti Wahitimu 33 kwenye shahada ya uzamili na mhitimu mmoja kwenye shahada ya uzamivu Stephen Mshana (mbele).

Kwaya ya kanisa katoliki kigango cha Bugando iliweka nakshi katika siku hii nzuri ya kumbukumbu.

Derick David, Magdalena Denis, Mamwanda Jebby, na Veronica Lyandala ni kati ya wahitimu 144 wa shahada ya udaktari (MD) waliotunukiwa shahada zao leo katika viwanja vya Hospitali ya Bugando jijini Mwanza.

Picha maalum ya meza kuu na Dr. Stephen Mshana (wa tatu toka kulia) mhitimu pekee aliyetunukiwa shahada ya uzamivu (PhD) toka Chuo cha Sayansi za Afya Bugando.

Jumla ya wahitimu 149 wametunukiwa stashahada na shahada mbalimbali, kati ya wahitimu hao wahitimu 51 ni wanawake.

Mtunukiwa Stashahada ya Udaktari wa magonjwa ya binadamu Dr. Mwandu Makani akiwa na ndugu zake waliokuja kumpa tafu la chereko kwenye maafali hayo.

picha ni habari ni kwa hisani ya gsengo.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA