FIFA YAFUTA RASMI UCHAGUZI TFF, YAWAPA ‘LIGHT GREEN’ MALINZI, WAMBURA WAGOMBEE

Rais wa TFF Leodgar Tenga.

Na Saleh Ally.
Shirikisho la soka la Kimataifa (FIFA) limetaka kuanzwa upya kwa utaratibu wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Uamuzi huo wa FIFA, maana yake mchakato huo utaanza upya unawaruhusu wote walioondolewa awali kama Jamal Malinzi na Michael Wambura kuwa huru kugombea tena.

Malinzi (kulia)
Pamoja na hivyo FIFA imeitaka TFF kuanzisha chombo kitakachoitwa kamati ya maadili na hadhi kwa ajili ya kusimamia mchakato huo.

Awali FIFA ilizuia uchaguzi huo ambao ulipangwa kufanyika February mwaka huu baada ya kukumbwa ba migogoro, lakini baada ya kufanya mahojiano na shirikisho hilo, wagombea pamoja na kamati mbalimbali (FIFA) wametoa maagizo hayo.


Akizungumza na waandishi wa habari hivi punde, Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema FIFA wamewaeleza kuna kasoro kati zilizojitokeza huku wakisisitiza kuundwa kwa kamati ya maadili na hadhi kabla ya Octoba mwaka huu.

Wambura.
“FIFA wamesema kuwa kuna sehemu tulikuwa tunakosea, tunatakiwa kuunda kamati ya maadili na hadhi ambayo itakuwa na mwanasheria ndiyo tuweze kuendesha uchaguzi huu.

“Wamepatupa muda hadi Oktoba na mchakato wote unaanza upya, wanaotaka watalipia fomu upya na kila kitu kwa sasa kitakuwa kipya kabisa,” alisema Tenga.

“Kwa kuwa mchakato utaanza mapema, Fifa wameomba tutengeneze taarifa ya mambo yanavyokwenda kabla ya Octoba ili kuokoa muda kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.”

Maana yake, Tenga aliyekuwa amemaliza muda wake zaidi ya miezi mitano iliyopita, ataendelea kuula katika nafasi hiyo akishughulikia maandalizi ya uchaguzi.

Uamuzi wa FIFA kuunda kamati hiyo, unaonyesha umelenga kufanyika kwa mchakato upya, lakini bado inaonekana kutakuwa na ugumu kwa baadhi ya wagombea kama suala lao litafikishwa katika kamati hiyo ya hadhi na maadili itakayokuwa imeundwa na TFF

SOURCE: www.gsengo.blogspot.com 

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA