TANGAZO KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA


Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania anapenda kuwatangazia watu 
wote wanaotaka kufanya Mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE) mwezi, Mei
2014 kama Watahiniwa wa Kujitegemea kwamba kipindi cha usajili kitaanza 
rasmi tarehe 1 Julai, 2013 kwa ada ya Shilingi 35,000/=. Kipindi cha malipo 
bila adhabu kitaishia tarehe 31 Agosti, 2013. Kuanzia tarehe 1 Septemba,
2013 hadi tarehe 30 Septemba, 2013 waombaji watajisajili kwa ada ya 
Shilingi 50,000/- (ada pamoja na faini).

Waombaji wote watajisajili kwa njia ya mtandao kupitia tovuti:
www.necta.go.tz. ya Baraza la Mitihani la Tanzania. Kabla ya kujisajili 
kwenye mtandao waombaji watapaswa kwenda kwenye vituo vya mitihani 
kuchukua namba rejea (reference number) watakazotumia kujisajili. 

Hakuna mtahiniwa atakayeweza kujisajili bila kupata namba rejea kutoka katika kituo 
anachokusudia kufanyia Mtihani. Wakuu wote wa vituo nchini watakabidhiwa 
namba rejea hizo kabla ya muda wa usajili kuanza na watazigawa kwa 
watahiniwa tarajali bila malipo.
IMETOLEWA NA:
KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA MITIHANI LA TANZA

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA