Skip to main content

Mvua yasababisha mafuriko Moshi vijijini, Mbunge Lucy Owenya awafariji waathirika

 

E86A6621
Mbunge wa viti maalumu, Lucy Owenya (Chadema) (kulia) akiwa ameongozana na diwani wa kata ya Arusha Chini, Rojas Mmari alipotembelea kujionea athari zilizotokana na mafuriko hayo.
Mafuriko makubwa yamevikumba vijiji saba kikiwemo kiwanda cha sukari cha TPC na kuathiri miundombinu pamoja na makazi ya watu kujaa maji.

Mbunge Lucy Owenya akitizama sehemu ambayo wananchi walilazimika kuibomoa kwa kushirikiana na uongozi wa kiwanda cha TPC ili kuruhusu maji kupita.
Mbunge Lucy Owenya akitembelea maeneo yaliyoathirika na mafuriko hayo.
Eneo lililobomolewa ili kuruhusu maji ya mafuriko kupita.
Baadhi ya nyumba zilijaa maji hali iliyowalazimu wahusika kutoa itu vya ndani nje.
Wengine walilazimika kuweka vyakula juu ya
mabanda ya kuku.
Baada ya maji kujaa wengine walilazimika kuhamishia magodoro yao juu ya paa la Choo.
Hata vyakula ambavyo vingi vyao vililowa na maji vilianikwa juu ya paa.
Mbunge Lucy Owenya akitizama namna ambavyo baadhi ya wananchi walivyoamua kuokoa vitu ya kwa kuianika juu ya paa.
Mifugo pia liathirika na mafuriko hayo.
Kutokana na hali hiyo Mbunge Lucy Owenya alilazimika kutoa msaada wa chakula kwa waathirika wa mafuriko hayo.
Mbunge Lucy Owenya akimfariji mmoja ya waathirika wa mafuriko hayo aliyekuwa akilia kwa uchungu baada ya kupoteza vitu vyake mbali,mbali ikiwemo vyeti vya taaluma ya utabibu.
Mbunge Lucy Owenya akikabidhi msaada wa chakula kwa wananchi walioathirika na mafuriko hayo.
Mbunge Lucy Owenya akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo.
Diwani wa kata ya Arusha Chini Rojas Mmari akizungumza jambo mara baada ya wananchi wake kukabidhiwa msaada huo.
Afisa mtendaji Utawala wa kiwanda cha sukari cha TPC ,Jafary Ally akizungumza kuhusu namna mafuriko hayo yalivyo athiri kiwanda hicho.(Picha zote na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini).

CHANZO:MO BLOG

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA