TIGO, MGAHAWA WA SAMAKI SAMAKI WAINGIA UBIA

Meneja wa Huduma za Masoko Tigo, Olivier Prentout (kushoto) akiongea na wanahabari wakati wa kusaini mkataba wa ushirikiano wa kibiashara kati ya kampuni ya simu za mkononi ya Tigo na Mgahawa wa Samaki samaki. Kulia ni Afisa Mkuu wa Maendeleo wa Mgahawa Samaki samaki, Saum Wengert.
Meneja wa Huduma za Masoko wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Olivier Prentout (kushoto) akiwa na Afisa Mkuu wa Maendeleo wa Mgahawa wa Samaki samaki, Saum Wengert wakionyesha mkataba wa ushirikiano wa kibiashara waliosaini kati ya kampuni ya Tigo na Mgahawa huo kwa waandishi wa habari jana jijini Dar Es salaam. 
Kampuni ya simu inayoongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali ya Tigo Tanzania, leo imeingia   ubia na mgahawa ya Samaki Samaki  ambao ilianzishwa tangu  mwaka 2007  ukiwa na matawi matatu  yaliyopo Mlimani City, City Centre na Masaki Jijini Dar es salaam,  ambapo pande hizo mbili zimekubaliana kufanya kazi pamoja  kwa kuleta  bidhaa/huduma zao kwa wateja wa kila mmoja.
 Akitangaza ubia huyo jijini Dar es salaam leo, Meneja wa Huduma za Masoko wa Tigo Oliver Prentout aliviambia vyombo vya habari kuwa ushirikiano huo  ni moja ya alama ambazo zinajenga imani  kwamba wateja wa Tigo ambao sasa wanaweza kujitambulisha  kupitia migahawa ya Samaki Samaki Tigo imeweka  mtandao wa 4G LTE kwenye migahawa yote yaSamaki Samaki ili kuwawezesha wateja  wake kufurahia  intaneti ya kasi na ya haraka wakati wakila  na kunywa  kwenye migahawa hiyo inayouza vyakula  vinavyotokana na mazao ya baharini hapa nchini.
“Tunaamini ushirikiano wetu  utandelea kuonesha ni jinsi gani tumejikita  kwenye kuboresha  mabadiliko kwenye mtindo wa maisha ya kidijitali na kuongoza kwenye kutoa  teknolojia ya kisasa  na ubunifu kwa wateja wetu, alisema Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez. 
 Aidha Muasisi na Mkurugenzi wa migahawa ya Samaki Samaki, Bw. Carlos Bastos alisema  Samaki Samaki wanawafanyia kazi Watanzania  na wameungana na Tigo  ambayo ni kampuni ya simu inayooongoza kwa ubunifu  nchini kuwapatia wateja wake   kile ambacho wamekisubiri kwa muda mrefu kwa jinsi huduma za Tigo  zilivyo  hususani uzoefu kwenye mtandao wa bure na wa kasi wa  intaneti.
Kwa ushirikiano huu  tutawapatia wateja wetu  miradi mingi mipya, maboresho  pamoja na ofa. Kufanya kazi na Tigo sio kwamba kunahusu  sisi kupata fedha tu, bali inahusu  ni nini cha ziada tunachoweza kuwapatia wateja wetu na hali kadhalika  ni kwa kiasi gani tunaweza kujifunza  kufanya kazi pamoja  na kampuni iliyo na uzoefu mkubwa na ya kimataifa.
Tunaweza kuwa ni  mgahawa unaoongoza kwa vyakula  vinavyotokan na mzao ya baharini, lakini  tunapenda kufanya  jambo zaidi kwa ajili ya wateja wetu. Huduma za Tigo zinazotarajiwa kuwepo  kwenye migahawa ya Samaki Samaki ni pamoja  huduma ya bure ya intaneti  bila nyaya (WiFi), Tigo Pesa na Tigo Music.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA