UGANDA YAFUTA SHERIA DHIDI YA USHOGA.

Wanaume wanaounga mkono mapenzi ya jinsia moja Uganda
Nchi ya Uganda ambayo ilidiriki kusimama kidete kupinga mapenzi ya jinsia moja hatimaye wameifuta sheria dhidi ya ushoga, ni maswali mengi watu watajiuliza je ni kwa sababu ya vikwazo vya nchi za Magharibi ambavyo viliwekwa baada ya Uganda kupitisha mswada huo na kuwa sheria. Mwandishi wa BBC anaelezea hali ilivyokuwa mpaka kufuta sheria hiyo.
Mahakama ya kikatiba nchini
Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja ambayo
ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada.
Mahakama ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni kinyume na sheria.

Baadhi ya waandamanaji waliounga mkono serikali kwa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja.
Mataifa kadhaa ya Magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.
chanzo bbc swahili
Comments
Post a Comment