TATIZO LA MIKOPO KUPATIWA UFUMBUZI


TANT1

Wananchi mbalimbali wakiingia katika Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa kwa ajili ya kujipatia bidhaa mbalimbali.Maonyesho hayo yameanza jana hii Jijini Dar es salaam.Picha n Daudi Manongi,MAELEZO

TANT01

Askari wa JKT pamoja na FFU wakihakikisha usalama wakati wananchi wakiingia katika viwanja vya Mwalimu Nyerere kuangalia bidhaa mbalimbali baada  ya maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa kuanza jana jijini Dar es salaam.
TANT3

Afisa Habari Idara ya Habari,MAELEZO Bi.Immaculate Makilika akizungumza jambo na Afisa Biashara kutoka Wizara ya Viwanda ,Biashara na Uwekezaji Bw.Baruti Mwaigaga(kushoto)  katika banda la Wizara hiyo viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

TANT4
Mwananchi akiangalia moja ya bidhaa  zinazotengenezwa na kikundi cha African Flowerless fashioncha Arusha kinachouza bidhaa zake nje ya nchi.Kulia ni Afisa wa kikundi hicho Bi.Suzana Mwalongo.
TANT5
Mafundi wakiendelea na upakaji rangi katika banda la CRDB katika Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar e Salaam.

Na: Immaculate Makilika- MAELEZO, Dar es salaam.
SERIKALI kupitia Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imeandaa mkakati ya kulipatia ufumbuzi tatizo la ukosefu wa mikopo linalowakabili wafanyabiashara wengi nchini ili kusaidia uanzishwaji wa viwanda.
Hayo yamesemwa na Afisa Biashara wa Wizara hiyo Bw. Baruti Mwaigaga wakati akizungumza katika Viwanja vya  Mwl Nyerere wakati wa maonesho ya Sabasaba yaliyoanza leo jijini Dar es Salaam.

“Kufuatia kuwepo kwa tatizo kubwa la upatikanaji wa mikopo kwa watu wenye nia ya kuanzisha viwanda hapa nchini, Serikali imeandaa utaratibu maalumu wa kutoa taarifa zinazohusu upatikanaji wa mikopo ili kusaidia wananchi, kitu ambacho hakikuwepo awali” alisema Bw. Mwaigaga
Alisema lengo la mkakati huo ni kumrahisishia mwananchi mwenye nia ya kuanzisha kiwanda kupata taarifa sahihi ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kupata mkopo ambao unaondoa usumbufu kwa walengwa ikiwa ni utekelezaji wa nia ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.

Mikakati mingine ya Serikali katika kukuza sekta ya viwanda nchini ni pamoja na kuanzisha programu ya kuendeleza viwanda vidogo vidogo katika mikoa ya Ruvuma, Pwani, Iringa, Tanga na Manyara.
Naye, Afisa Uchumi kutoka Wizara hiyo Bw. Vicent Turuka alisema katika kutekeleza azma ya Serikali ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda, Wizara inawaunganisha wafanyabiasha wadogo wadogo na wanunuzi wakuu na kuwapatia masoko ya mazao mfano zao la ufuta lina soko kwa kampuni ya Oramu pamoja na Murza Mills.

Aidha, wananchi wamesisitizwa kutembelea banda la Wizara ya Viwanda na Bishara  pamoja na taasisi zake za BRELA, TBS, TFDA , CBE na SIDO lililopo katika viwanja hivyo vya maonesho ili kupata taarifa mbalimbali kuhusu namna za kufanya biashara pamoja na kuanzisha viwanda nchini

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA