MWANAMKE ALIYEKATAA KUOLEWA ACHOMWA HADI KUFA PAKISTAN


Mwanamke mmoja wa Pakistan aliyechomwa kwa kukataa wito wa ndoa amefariki kutokana na majeraha yake.
Maria Sadaqat ,mwalimu wa shule aliye na umri mdogo alishambulia nyumbani kwake na kundi moja la wanaume siku ya jumapili na kufariki katika hospitali mjini Islamabad siku ya Jumatano.
Familia yake imesema kuwa alikataa kuolewa na mtoto wa mmiliki wa shule ambayo amekuwa akifunza.
Wanakampeni wanasema kuwa visa vya mashambulio dhidi ya wanawake wanaokataa kuolewa ni vingi nchini Pakistan.
Waziri mkuu wa Punjab Shahbaz Sharif alianzisha uchunguzi kuhusu mauaji hayo.
Babake Maria amesema kuwa mmiliki wa shule hiyo ni mojawapo ya watu waliomshambulia mwanaye.
Polisi wameambia BBC kwamba wanaume hao walimpiga kabla ya kumwagia mafuta ya petroli na kumchoma karibu na eneo la kitalii la Muree,karibu na mji mkuu.
BBC.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA