Man United yambakisha Rooney


wayne Rooney

MKURUGENZI wa Manchester United, David Gill, atakutana na Wayne Rooney, kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kuongeza katika klabu hiyo.

Wakati nyota huyo kabakisha miaka miwili katika mkataba wake, uongozi wa United, umepanga kumuongezea mkataba mchezaji huyo.

Juzi, United, ilitangaza kukubaliana na Nemanja Vidic, kubaki klabuni hapo kufuatia taarifa kuwa angeweza kuhamia Real Madrid au AC Milan.

Rooney, atafanya mazungumzo na United baada ya kurejea mapumzikoni na atakuwa mchezaji wa pili kusaini mkataba mpya na klabu hiyo.

"Mpango wa sasa ni kukutana na Wayne na washauri wake pindi atakaporudi likizo kwa lengo la kuzungumzia mkataba mpya,” Gill, aliwaambia waandishi wa habari.

"Aliwahi kusema na sisi tuliwahi kusema kuwa, tunahitaji kukutana na kulizungumzia suala hili, ili tuendelee kumpa maisha mapya hapa United.

"Ukiangalia malengo yake na jinsi anavyojituma katika klabu hii ni wazi mpango huu utafanikiwa."?

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA