BAADA YA MGOMO HATIMAYE DALADALA ZAREJEA KUTOA HUDUMA.

Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje akizungumza na madereva hao kuwasihi kurejea katika huduma kwani wananchi wanataabika.
Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Liberatus Barlow akiwataka madereva hao kurudi katika huduma kwani suala lao tayari limekwishafika katika vyombo husika.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa chama cha madereva wa daladala Kanda ya Ziwa Protas Dede, amewaomba radhi wananchi kwa hali iliyotokeza na usumbufu walioupata kwani imewabidi kuchukuwa hatua hiyo kwa dhamira ya kutetea haki yao ili mambo yaende sawa.
Dereva wa daladala akitoboa kero zake mbele ya wanausalama barabarani.
Sasa ni zamu ya mwanausalama..
Mwisho ikawa ligi...
Hivi ndivyo hali ilivyokuwa huku jeshi la polisi likiimarisha ulinzi eneo la kusanyiko viwanja vya Ghand Hall jijini Mwanza.
Usalama uliimarishwa kama kawa..
Haikujulikana ni nini kilikuwa kimewasibu wanafunzi hawa hata wakafungwa pingu za kamba wakielekea kituo cha polisi kati.
 
         picha na story nzima ni kutoka www.gsengo.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA