SSPRA WATEMBELEA HIFADHI YA SERENGETI

Wanachama wa SSPRA mwishoni mwa wiki iliyopita siku ya Ijumaa tarehe 16/03/2012,kuanzia majira ya saa 2 asubuhi walianza safari yao ya kuelekea katika hifadhi ya taifa ya Serengeti (SENAPA) Katika kujifunza mambo mbalimbali yanayoendana na taaluma wanayosomea ya Uhusiano wa Umma na Masoko.(Public Relations and Marketing),pia katika kuendeleza sera ya utalii wa ndani ambayo imekuwa ukilegalega sana hapa nchini.

Safari hii imekuwa yenye mafanikio makubwa sana kwani kila kitu kilichokuwa kimepangiliwa na kamati ya Mafunzo ya nje kwa vitendo chini ya Mwenyekiti Bw.Mshana Shaabani imeweza kutekelezeka vizuri sana . Wanachama wameweza kujifunza mambo mengi sana ambayo hawakuwa wakiyafahamu kutoka kwa Afsa utalii Bw. Fred Shirima kama vile historia halisi ya Serengeti,umuhimu wa hifadhi ya Serengeti kwa Tanzania na dunia nzima,sifa za hifadhi ya Serengeti iliyonayo, vivutio vya kipekee vinavyopatikana katika hifadhi hii pekee, na pia changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika utendaji wa kazi za uhifadhi. Pia Bw. Sadati Kimaro ambaye alikuwa ni mwongozaji wa safari (game driver) wakati wote ndani ya hifadhi alitoa maelezo mbalimbali yanayohusiana na wanyama hakuchoka kujibu maswali yote pindi alipokuwa akiulizwa na wanachama wa SSPRA.
Uongozi wa SSPRA unapenda kutoa shukrani zake za dhati kabisa kwa Uongozi wa hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa kuitikia ombi la SSPRA, Uongozi wa chuo kikuu cha Mt.Augustino kupitia idara ya uhusiano wa umma chini ya mkuu wa idara Cezalia B. Mwidima, wadhamini wa safari kampuni ya SBC Company Limited (Pepsi), Mukeshi travels, pia mlezi wa SSPRA Bw.Albert Tibaijuka.
Zifuatazo ni baadhi ya picha zilizochukuliwa wakati wa safari,pia Video itakuwepo baada ya kumaliza kuifanyia editing.
Maelekezo hayakukosekana

Wanachama wa SSPRA wakiwa kwenye mkutano,wakimsikiliza Afsa utalii Bw.Fred Shirima
baada ya kikao wanachama wakapata picha ya ukumbusho mahali hapa
Wadhamini wa Safari yetu pia tukawashukuru
Hao ni wanachama wa SSPRA wanaosoma mwaka wa tatu
Bwana.Fred Shirima ambaye ni Afsa Utalii akitoa maelezo juu ya serengeti

Simba akiwa amepumzika juu ya mt,hapa tulifurahi sana baada ya kumwona
Mnyama mwenye maringo kuliko wote ndani ya hifadhi
Members wakiwa hotel ya Seronera








Geti la kwanza la Ndabaka,hapa kabla ya kuingia ndani ya Hifadhi









kuchimba dawa pia kulihusika


Hayo sio mawe,ni viboko mahali hapa tulishangaa sana panajulikana kama hippo pool







Siku ya kwanza kabisa kufika mahali tulipolala,panaitwa Youth Hostel











Game driver Sadati Kimaro na Nyanja Poti wakiwa wamepozi pia



















Comments

  1. Good job SSPRA n that how the PR should be,tumeusahau utalii wa ndani kwa muda mrefu...vivutio ni kwa ajili yetu sio wazungu pekee yao!!

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA