TWANGA PEPETA KUWAPA BURUDANI WAKAZI WA MUSOMA

Bendi ya Muziki wa Dansi ya Twanga Pepeta imepania kukonga nyoyo za wapenzi wa bendi hiyo na wapenzi wote wa Muziki Mjini Musoma siku ya Ijumaa ya Machi 31 pale watakapofanya onyesho lao la kwanza Mjini hapa baada ya kufanya hivyo takribani miaka 3 iliyopita.

Akizungumza na mwakilishi wa blog hii kutoka Musoma Bwana Shomari Binda kwa njia ya simu wakiwa njiani kuja Musoma,mratibu wa ziara hiyo ambayo ni maalumu kwa wakazi wa Kanda ya ziwa Martin Sospeter amesema kuwa wamefanya maandalizi ya kutosha kwa muda wote ili kuhakikisha wanatoa burudani ambayo itakidhi haja kwa wale wote watakaobahatika kufika kuangalia onyesho la bendi hiyo.

Amesema katika ziara hiyo wataitambulisha Album yao mpya inayokwenda kwa jina la Dunia Daraja ambapo ndani yake kuna nyimbo kama vile Mapenzi hayana kiapo,Penzi la Shemeji,Mtoto wa Mwisho pamoja na nyingine zilizomo katika Album hiyo.

Martini amesema kuwa licha ya kupata Burudani ya nyimbo mpya za Bendi hiyo,wapenzi wa Twanga Pepeta pia watapata ladha ya vibao vya zamani vya Bendi hiyo vilivyopata kutamba ambavyo vitaongozwa kuimbwa na mwanamuziki mkongwe hapa nchini ambaye amejiunga tena na bendi hiyo Mwinjuma Muumini(Kocha wa Dunia).

Amesema kuwa licha Muumini na wanamuziki wengine wa bendi hiyo wameongozana na mshindi wa kwanza wa mashindano ya Bongo Star Sarch (BSS)mwaka 2011 Haji Ramadhani ambaye pia ampania kutoa burudani ya kutosha kwa wakazi wa Musoma ikiwa kama shukrani ya kumpigia kura na kuibuka mshindi wa kwanza katika mashindano hayo yaliyowakutanisha mastaa kibao.

Ameongeza kuwa burudani hiyo ya Twanga Pepeta itafanyika katika ukumbi wa Musoma Club kwa kiingilio cha shilingi elfu kumi (10,000) huku burudani hiyo ikipangwa kuanza majira ya saa2 usiku a tayari maandalizi yote katika ukumbi huo yamekwisha kukamilika na kinachosubiliwa ni kwa wapenzi wa bendi hiyo kwenda kulicheza Twanga.
habari imeandaliwa na mwakilishi wa blog hii kutoka Musoma Bwana Shomari Binda.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA