SINA MAHUSIANO NA SITTI MTEMVU- LUDENGA


Mkurugenzi wa Lino Agency ambao ni waandaaji wa MISS Tanzania, Hashim Lundenga amefunguka na kuweka wazi kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na aliyekuwa mshindi wa kwanza wa Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu.

Mkurugenzi wa Lino AGENCY akichat LIVE na mashabiki wa EATV kupitia ukurasa wa facebook wa EATV
Lundenga amefunguka hayo leo alipokuwa akichata LIVE kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa sita mchana mpka saa nane mchana.
Mbali na mahusiano Watu wengi walitaka kujua ni sifa zipi zilizompelekea mrembo Sitti Mtevu kutwaa taji hilo kama si upendeleo kutoka katika kamati na crew inayohusika kuandaa mashindano hayo kwani watu wengi wamekuwa wakisema kuwa mrembo huyo alikuwa hastahili kushinda taji hilo ukilinganisha na warembo wengine ambao walikuwa wakichuana nae,kufuatia hali Ludenga ikabidi aweke wazi sifa tano amabzo zinamfanya mtu kushinda taji la MISS Tanzania kuwa ni lazima awe na sura nzuri, umbo zuri, mvuto, haiba, ufahamu wa kutosha wa mambo mbali mbali.
SITI HANA SIFA YA KUWA MISS TEMEKE
Kutokana na maamuzi ambayo Sitti Mtevu aliamua kujivua taji la Miss Tanzania 2014 hivyo mrembo huyo amejifutia sifa zake zote alizopata katika kusaka taji la Miss Tanzania hivyo si Miss Chang'ombe wala si Miss Temeke tena.
Hashim Lundenga amesema kuwa kitendo cha Sitti kujivua taji hivyo automaticaly amevua mataji yake yote aliyopata katika ngazi ya wilaya mkoa na hata Taifa kama ambavyo ilivyotangazwa.
"Hashim Lundenga: Automatimacally anakuwa amejivua na mataji mengine pia...."
Kufuatia sakata la Mrembo Sitti Mtevu kudanganya UMMA juu ya umri wake na kumgharimu kulivua taji hilo la Miss Tanzania 2014.Ludenga amesema kuwa hali ya udanganyifu wa umri wa warembo hao huwa ni suala la kawaida na lipo kila mwaka ila kwa kuwa huwa wako makini ndiyo maana wangundua hivyo haoni sababu ya yeye na kampuni yake kuwajibika kisa Sitti Mtevu alidanganya umri.
"Hashim Lundenga: sio sahihi, tupo makini na ndio maana tumegundua, fahamu ya kwamba kila mwaka washiriki wengi tu hutudanganya kuhusu umri wao na ndio maana tupo makini...... tuwajibike kwa kosa gani?????"
NIPO TAYARI KUKABIDHI KIJITI KWA MWINGINE
Kufuatia kuzuka kwa kashfa mbalimbali zinazohushisha mashindano ya Miss Tanzania na waandaaji wake mashabiki wa Eatv walitaka kujua kama Mkurugenzi huyo wa Lino Agency Hashim Lundenga yupo tayari kuachia nafasi hiyo ili watu wengine waweze kuendeleza pale wao walipohishia lakini Ludenga aliweka wazi kuwa yeye kama Mkurugenzi yupo tayari kuchagua mtu mwingine ili asimamie nafasi yake lakini si kuwaachia watu wengine kuendesha shindano hilo.
"Hashim Lundenga :Lino International Agency ni Kampuni ya mtu binafsi na inayo Directors wake, hivyo tunaweza kuteua Mkurugenzi mwingine wa kufanya kazi hiyo........"
MISS TANZANIA HAIWEZI KUFUTWA
Kutokana na baadhi ya watu kutooana umuhimu wa uwepo wa mashindano ya Miss Tanzania na kuyahusisha na kumomonyoka kwa maadili hususani kwa warembo wa Tanzania watu wamependekeza mashindano hayo yafutwe kwani yamekuwa hayana tija na hayana haki kwani kumekuwa na upendeleo na udanganyifu na vitendo vya rushwa ambavyo hupelekea wasichana wengi kuvunja utu wao kwa sababu ya kutaka kushinda au kufikia hatua fulani katika mashindano hayo.
"Hashim Lundenga:Sitty bado ni msichana mrembo na ataendelea kuwa mrembo....haya mashindano hayawezi kufutwa kwa sababu wananchi wanaelewa faida zake, wewe usiyejua faida zake, baki hivyo hivyo..."
MISS TANZANIA HAKUNA FAIDA YOYOTE
Hashim Lundenga ameweka wazi kuwa katika mashindano hayo hakuna faida yoyote anayopata zaidi ya yeye mwenyewe kufahamika na kutembea nchi nyingi duniani,watu walitaka kujua kwanini miaka yoye amekuwa aking'ang'ana yeye tu katika kuandaa na kusimamia mashindano hayo na je anafanya kwa masilahi ya nani na hayo ndiyo yalikuwa majibu ya Lundenga
"Hashim Lundenga hakuna faida yeyote, zaidi ya kufahamika, kutembea nchi nyingi duniani, n.k."
KASHFA YA NGONO KWANGU FITINA TU
Hashim Lundenga amekana leo wakati akichat Live na mashabiki wa ukurawa wa EATV kuwa hana kashfa ya kuomba ngono au kuwa lazimisha warembo hao kutoka na yeye kingono ili waweze kushinda au kushiriki mashindano hayo,Ludenga anasema hizo ni fitina tu za watu fulani wenye lengo la kumchafua na kuchafua mashindano hayo.
"Hashim Lundenga hakuna kashfa kama hiyo..........hiyo ni fitna.............."
Lakini pia Lundenga aliwaambia watanzania kuwa kutokana na Sitti kujivua taji na kumpa nafasi mshindi wa pili kuchukua taji hilo hivyo wasitegemee tena sherehe za kumkabidhi taji hilo Miss Tanzania namba mbili kwani shehere watafanya wazazi wake pamoja na wakala wake wa mkoa alipotokea
"Hashim Lundenga hakuna sherehe yeyote, sherehe huandaliwa na wazazi wake na wakala wake wa mkoa alipotokea"
Hashim Lundenga alimaliza kwa kusema kuwa tunaoomba radhi sana kwa wale wote ambao hatukuweza kujibu maswali yenu yote kutoka na ufinyu wa muda.
CHANZO : EATV

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA