DIAMOND PLATNUMZ ABEBA TUZO TATU KATI YA NNE ZA CHOAMVA14 HUKO AFRIKA KUSINI


Diamond Platnumz ameiwakilisha vema nchi ya Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla katika tuzo za CHOAMVA 14 zinazoandaliwa na kituo kikubwa cha runinga cha Channel O kilichopo nchini Afrika kusini. Diamond ameweza kuondoka na tuzo tatu usiku huu kati ya nne alizokuwa akiwania, tuzo alizoshinda ni Most gifted East African, Most gifted new comer na Most gifted Afro Pop. Tuzo ambayo ameikosa imenda kwa mwanamuziki Doc Shebeleza inayojulikana kama Most  gifted video of the year.




Katika tuzo hizi Diamond ameongozana na mama yake mzazi Bi sandra, pamoja na Management yake akiwepo babu Tale na Mkubwa Fela, lakini kilichokuwa cha kuvutia Zaidi na kutawala mazungumzo mengi katika mitandao ya kijamii ni baada ya kumuona mwana dada zaritheboss kutoka Uganda akiwa ameambatana naye na kupiga baadhi ya picha huku Zari akiwa na mama Diamond kwenye gari la kifahari, watu wamezidi kujiuliza maswali je ndo ile project aliyoisema kwenye vyombo vya habari bado inaendelea? Kwani katika kutoa shukurani zake wakati wa tuzo alimshukuru fans wake waliopo duniani kote,mama yake,uongozi unaomsimamia na  baby wake.
Kupitia account ya Instagram ya Wema Sepetu amepost picha hii kwa chini ikiambatana na maneno haya“Gnyt Instagramers…And Hongera tele ziende kwa kaka Platnumz…..I must say he did Tanzania proud” hapo kwenye neno kaka ndipo haswa panaibua swali.


Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA