Kinachompa jeuri Mourinho dhidi ya Wenger kipo hapa

Mourinho_Wenger_he_3394228b
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho ameingia tena kwenye headlines kwa kauli zake anazozitoa kuelekea mchezo wa Ngao ya Hisani, Chelsea itakutana na Arsenal leo August 2 saa 11 jioni kwenye uwanja wa Wembley wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 90,000.Mourinho ambae anajulikana kwa kuwa na uwezo wa kucheza na akili ya kocha wa timu pinzani amerudi na kauli nyingine dhidi ya Wenger.
download
“Sifikirii kuhusu nini kilitokea nyuma, nafikiria kuhusu mechi mimi kushinda mechi sita, saba, nane au tisa bila kupoteza mechi hata moja haiweki utofauti wowote na sifikiri kama itasaidia chochote kwenye huu mchezo, mechi inayofuata kwangu haina mahusiano yoyote na mechi iliyopita “>>>Mourinho
Mourinho_presser_3394231b
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger hajawahi kuifunga klabu ya Chelsea hata mara moja ikiwa chini ya Jose Mourinho, wachambuzi wa masuala ya soka wanatafsiri kauli zaMourinho kama ni njia ya kumdanganya kocha wa Arsenal Arsene Wenger ili ajiamini zaidi.
wengervsmourinho1
Mourinho amekuwa na rekodi nzuri dhidi ya kocha wa Arsenal kwani akiwa na kikosi cha Chelsea amewahi kucheza na Arsenal mechi 12 na kushinda mechi saba na kutoka suluhu mechi tano hivyo hiyo ni sababu inayoendelea kumtia jeuri
chanzo:millard ayo

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA