MKUU WA WILAYA AAGIZA WALIMU WAKUU WASHUSHWE VYEO

17 Feb2015


Zaidi ya watu hamsini wamekamatwa na jeshi la polisi kufuatia vurugu kubwa iliyotokea katika mji wa Katoro mkoani Geita.

Chanzo cha vurugu hizo ni mgomo wa wanafunzi wa shule za msingi Kilimani, Mkapa na Ludete ambapo walilala katikati ya barabara, kushinikiza kuwekewa matuta kutokana na matukio ya ajali ya mara kwa mara hivyo kutishia usalama wao.

Hata baada ya kuwekewa matuta kuzuia ajali vurugu hizo zilipamba moto kutoka kwa wanafunzi na kuingia watu wazima na kuanza kupiga mawe magari yote yaliyokuwa yakipita barabarani na zaidi ya magari saba yameharibiwa vibaya na watu kujeruhiwa.

Baada ya muda kuonekana hali imetulia magari yaliruhusiwa kuondoka hata hivyo hali haikuwa shwari ambapo magari yote yalirudi kituo cha polisi Katoro kwa usalama zaidi.

Mkuu wa wilaya ya Geita ameagiza Walimu Wakuu wote wa Shule za Msingi zilizohusika na uanzishwaji wa vurugu hizo kushushwa vyeo vyao na hatua mbalimbali za kisheria zizingatiwe.

  • Taarifa ya ITV

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA