AGNESS MASOGANGE AMDATISHA MWANAUME WA SOUZ

Yule mwanadada, ambaye ni video queen na role model wa teenage girls katika ka nchi ka Tanzania tena anayekumbukwa na wengi kwa kusafirisha panadol zenye thamani ya bilioni 6 kwenda South Africa anatarajiwa kuolewa karibuni

Modo Agnes Masogange ameonekana kumdatisha mwanaume aliyefahamika kwa jina la Louis Donald wa nchini Afrika Kusini baada ya jamaa huyo kuposti mtandaoni picha tofauti akiwa amepozi kimahaba na Agnes na kueleza kuwa, huyo ndiye mke wake wa kufa na kuzikana.

Jamaa huyo amekuwa akieneza habari kuwa, Masogange ni ‘mtu’ wake kitendo kilicholifanya Ijumaa ambalo awali lilikuwa na taarifa kuwa, Agnes amechumbiwa na msanii aitwaye Evance Komu limtafute mrembo huyo ili afafanue na alipopatikana alisema:
“Hiyo ishu ipotezee bwana, maswali gani hayo unaniuliza?” alihoji Masogange aliyeonekana kutotaka kuweka wazi ishu zake za kimapenzi.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA